Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia katika hoja hii ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa viwanda katika Mkoa wa Njombe, kwa vile Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati wa Tanzania ya viwanda, naiomba iandae mazingira wezeshi na rafiki kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Njombe ili wawekeze katika viwanda. Tatizo kubwa ni kwamba inawabana sana wafanyabiashara kwa taratibu ngumu zinazosababisha watu waone vigumu kuanzisha viwanda. Pia zile hatua za uanzishwaji wa viwanda ni ngumu na ni ndefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa jokofu la kuhifadhia matunda (maparachichi), Mkoa wa Njombe unazalisha matunda ya parachichi kwa wingi lakini hakuna jokofu la barafu kwa ajili ya kuhifadhi matunda hayo. Naiomba Serikali itusaidie kutafuta fedha ya kununulia jokofu hilo au kupata mwekezaji mkubwa anayeweza kutufadhili jokofu hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa soko la mahindi; wakulima wa nchi nzima wanahamasika kulima mahindi kwa wingi lakini tatizo kubwa hakuna soko, mfano wakulima wa Mkoa wa Njombe walipata mahindi kwa wingi lakini mahindi hayo yanaoza. Naiomba Serikali ifungue mipaka ili wananchi wa Mkoa wa Njombe wauze mahindi yao nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.