Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira ya uwekezaji; niishauri Serikali kuangalia jinsi Serikali na watendaji kupunguza urasimu kwa wawekezaji kwani imefikia watu/wawekezaji wanahofia kuwekeza kutokana na sera zetu zinazobadilika mara kwa mara, hivyo kuhofia kupoteza mitaji yao. Pia nizungumzie tozo zilizopita kiasi mfano TBS, TFDA, OSHA vitu vyote hivyo badala iwe inalipiwa mahali pamoja na kuhakikisha kodi yake inakuwa ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu leseni la biashara; niishauri Serikali kuangalia mlolongo wa upatikanaji wa leseni. Unatakiwa kulipa TRA baada ya kukadiriwa kwa mteja ambaye ndio kwanza anaanza biashara atakadiriwa kwa mteja badala kwa faida baada ya biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, masoko ya uhakika; nizungumzie masuala ya masoko nishauri Serikali kuhakikisha inatafuta soko la bidhaa za watanzania kwani wanazalisha bidhaa lakini hakuna soko la uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali ijitahidi kutafuta masoko hata kwa bidhaa za viwandani kwani kuanzisha viwanda bila soko la bidhaa hizo itakuwa kama viuatilifu vya Kibaha ambavyo hakuna soko na uzalishaji imebidi kupunguzwa. Kutokana na kupungua uzalishaji kiwanda kimeshindwa kuajiri vijana wa Kibaha wa kutosha.