Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tafsiri na upotoshaji wa maana halisi ya viwanda vidogo. Tunaomba kupata tafsiri sahihi, maana ya viwanda na aina ya viwanda vinavyozungumziwa na Wizara husika ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo yana viwanda vingi na kuna maeneo ambayo hayana viwanda kabisa. Napenda kujua kigezo kinachotumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wawekezaji kukata tamaa ni vyema likaangaliwa upya kuhusiana na mazingira ya wawekezaji ili kukuza uchumi wetu. Aidha, ni vyema kama Taifa kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wetu wanaotaka kuwekeza nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vyema umeme uwe na uhakika ili kuendesha viwanda na kuwapa wawekezaji nchini kuwa na uhakika na uwekezaji wao kwa kuwa kila mtu anawekeza ili apate faida, inapotokea changamoto ya umeme na maji wawekezaji wanaweza kukata tamaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uanzishwaji wa kiwanda cha dawa ni muhimu sana kwani kukiwa na viwanda vingi vinavyozalisha dawa za binadamu kutasaidia Taifa na wananchi wa kawaida kwani bei itakuwa nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu kuanzisha Kiwanda cha Mbolea. Mbolea inahitajika sana nchini lakini kumekuwa na changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kutolewa semina elekezi kwa wafanyabiashara na TRA juu ya kulipa kodi badala ya hii hali ambayo inajitokeza sasa kwa kuonekana uadui mkubwa kati ya wafanyabiashara na TRA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya sasa kiuchumi katika nchi yetu ni tete mno hasa kwa wananchi wa chini kabisa. Ni vyema kukawa na mazingira rafiki kwa wafanyabiashara wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wafanyabiashara kuhama kutokana na changamoto wanazokutana nazo Serikali iweke utaratibu mpya utakaosaidia wafanyabiashara wetu.