Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukaguzi wa TBS, NEMC, TFDA; Serikali kupitia mamlaka mbalimbali imekuwa ikifanya ukaguzi wa maeneo ya viwanda, bidhaa za viwanda na kutoa vibali au kuteketeza mali za wajasiriamali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa la mamlaka hizi ni rushwa, urasimu na kutumia standards za Ulaya kwa kuwafanya Watanzania wengi kukwama kuanza biashara, kuchelewa kuanza biashara na kufilisika kutokana na matumizi mabaya ya sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali kama tunataka viwanda viongezeke, nchi yetu lazima iondoe rushwa, urasimu na Europe Standards kwenye vigezo vya kufanya biashara au ubora wa bidhaa za Watanzania. Kwa sababu duniani kote kuna export quality na kuna internal consumption quality, lazima tuondoe masharti yanayokwamisha kuanza biashara na kujenga viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kutumia TIC imekuwa ikihamasisha wawekezaji kutoka nje kuwekeza Tanzania. Wawekezaji wengi wanaokuja na mitaji yao na kununua ardhi na kumiliki kwa asilimia mia moja; nchi kabla ya kuingia kwenye mkakati huu wa viwanda haikuandaa sera itakayolinda wazawa na kuzuia utoroshaji wa faida zote kwenda nje. Mfano, viwanda vyote vikimilikiwa na wageni, maana yake faida yote ya uwekezaji mkubwa itakwenda kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni kwamba tulitakiwa kuwa na sera ya kulinda maslahi ya nchi ili kuepuka matatizo tunayopata sasa kwenye uwekezaji mkubwa wa madini kumilikiwa na wageni watupu na kuruhusu wizi mkubwa, udanganyifu mkubwa kupitia transfer pricing na cheating kwenye contracts?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kutazama upya Sera ya Uwekezaji kwenye viwanda ili kuruhusu mgeni kuuza sehemu ya haki zake kwa wazawa, suala ambalo litasaidia kupunguza profit export kurudi kwao na kuiacha Tanzania maskini.