Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipatia fursa ya kuhitimisha hoja ya Wizara yangu. Hoja zangu ziko kwenye makundi makuu mawili, kundi la kwanza ni hoja kama zilivyowasilishwa na Wabunge kupitia kwenye Kamati inayosimamia Wizara hii, niwashukuru kwa kuleta hoja zao na ninawaahidi kwamba nitazitekeleza. Kundi la pili ni Waheshimiwa Wabunge ambao ama walizungumza ama walikuja kwa maandishi wakichangia bajeti hii. Waheshimiwa Wabunge 50 wameweza kuchangia kwa kuongeza hapa Bungeni na Waheshimiwa Wabunge 39 walichangia kwa maandhishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi Mheshimiwa Spika wakati alipokuwa hapa nawasilisha alitupa dira na nadhani ndiye aliyewapa hamasa Waheshimiwa Wabunge kwamba muijenge upya, mui-shape upya hii bajeti. Hiyo yote yaliyosemwa nakwenda kuandika upya utekelezaji wangu wa mwaka unaokuja. Kwa kukubali kwangu huko niko mbele yenu nikiwaomba mpitishe bajeti yangu nitaitekeleza kama mlivyonishauri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongozwa na Dira ya Taifa 2020/2025 ambayo kama Taifa tunalenga ifikapo mwaka 2020/2025 Taifa letu liwe Taifa la uchumi wa kati. Uchumi wa kati Watanzania wenye kipato cha kati tungetamani Mtanzania wakati huo 2020/2025 awe na kipato kwa wastani wa dola 3,000, hicho ndicho kipato tunachokitaka ili kufikia hapo kwenye uchumi wa kati uliojumuishi chombo cha kutupitisha mpaka hapo ni uchumi wa viwanda. Dira yetu ya Taifa inajengwa katika mipango mitatu ya miaka mitano mitano iliyoanza mwaka 2011 inayoisha 2026. Mpango wa kwanza ulilenga kuondoa vikwazo, mpango wa pili ni ujenzi wa uchumi wa viwanda na mpango wa tatu kujenga uchumi shindani (the capacitive economy).

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kufika hapo tunaongozwa na mkakati (Integrated Industrial Development Strategy) wa 2011 unakwenda mpaka 2020/2025 unaelelezea yote ambayo Waheshimiwa Wabunge mlikuwa mnanikumbusha yote yameandika mle. Huo ni mkakati mkubwa, ndani ya mkakati mkubwa kuna mkakati mdogo, mkakati mdogo wa kwanza unazungumzia kutoka pamba mpaka mavazi, mwingine unazungumzia fursa ya kutumia mafuta ya kula kutoka kwenye mbegu tuzalishayo hasa hasa alizeti. Kama mlivyosema Waheshimiwa Wabunge mafuta ya kula ni bidhaa ambayo inachukua pesa zetu za kigeni ikiwa namba mbili ikifuatiwa na mafuta ya jamii ya petroli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati mwingine kama mlivyosema Waheshimiwa Wabunge upo unazungumzia namna gani tutengeneze ngozi na bidhaa za ngozi. Wakati mwingine mdogo ni wa madawa, mkakati mwingine ni wa kujitosheleza chakula, mikakati yote hii inajengwa ndani ya mkakati mkubwa wa Integrated Industrial Development Strategy.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunapojenga uchumi wa viwanda kwa maandiko ya mipango hiyo mitatu na kwa maelekezo ya viongozi wakuu, tunaambiwa tulenge mambo matatu, tujenge viwanda ambavyo vinaajiri watu wengi. Tujenge viwanda ambavyo bidhaa zake zinatumika sana, lakini tujenge viwanda ambavyo vinategemea malighafi zinazozalishwa na Watanzania walio wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoeleza viwanda vinavyozalisha bidhaa zinazotumika kwa wingi tumebakiza item moja na mimi na Waziri wa Afya tumeweka kipaumbele kuhamasisha ujenzi viwanda vya madawa. Tutakapokuwa tumefanikiwa kujenga viwanda vya madawa sekta ya bidhaa zinazozalishwa kwa wingi tutakuwa tumevuka. Kama nilivyoeleza tunajitosheleza kwa nondo, lakini Mheshimiwa Bulembo amehoji inakuwaje nondo zinapanda bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika soko la dunia chuma kimepanda bei hatujafika Bajeti Kuu ya Serikali tutaangalia namna gani ya kufanya, lakini mtoto mzuri Dangote ambaye mimi namuita mtoto mzuri, alipoharibikiwa mitambo yake ya clinker kutokuwepo kwa Dangote ambaye yeye anazalisha tani milioni tatu kwa mwaka hawa wazalishaji wadogo wakashindwa kulihimili soko. Kwa sababu Dangote alipoleta industry shakeout hawa wazalishaji wengine walikuwa wamerudi nyuma wakizalisha kwa kujikimu, sasa alipoondoka kwenye soko tukabaki na vacuum, lakini Dangote wakati wowote atamaliza mtambo wake wa clinker na wakati huohuo anafungiwa gesi kila kitu tayari atarudi troublemaker, tuweze kurudi kwenye bei zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naelezea viwanda ambavyo bidhaa zake zinatumika kwa wingi ndiyo tuko hapa, tumebakiza madawa, pili tumebakiza mafuta ya kula ambayo nitaelezea suluhisho lake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachofanya siyo kufika uchumi wa kati, ni kufika uchumi wa kati ulio jumuishi na uchumi wa kati ulio jumuishi unaupata kwa kupitia viwanda vinavyotegemea mali za wakulima na ndiyo maana tunazungumza viwanda kuanzia vijijini, ndiyo maana tunazungumza viwanda vinavyochakata malighafi za wananchi, yule anayelima pamba anapata keki yake, anayeivuna anapata keki yake, anayeichakata kwenye ginnery anapata keki yake, anayetengeneza nguo anapata kipande cha keki na anayekwenda sokoni kuuza nguo ndiyo uchumi jumuishi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ilibidi niliendeleze hivyo, ili kujenda uchumi jumuishi ambapo Wizara yangu inakuwa ni kitovo na muhimili nahitaji watu wa kuniwezesha. Nichukue fursa hii kumpongeza Waziri wa Nishati amezungumza, bila nishati huwezi kujenga viwanda, unahitaji nishati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru Waziri wa Nishati umezungumza power mix sipaswi kuirudia, tunahitaji umeme wa kutosha. Hatuwezi kuuza mawese ya Kigoma, Kigoma inaweza kuzalisha mawese lakini soko liko Dar es Salaam, asilimia 50 mpaka asilimia 70 ya bidhaa zote ziliwazo Tanzania huliwa Dar es Salaam. Hivyo mawese ya Kigoma bila usafirishaji mzuri hamuwezi kuyauza Dar es Salaam, ndiyo maana tunajenga standard gauge, kumbe reli miundombinu wezeshi, barabara ni miundombinu wezeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mlivyosema bila maji hatuwezi kwenda popote, namshukuru Mwenyezi Mungu Bwawa la Kidunda litawezesha Bagamoyo Special Economic Zone na Dar es Salaam kufanya kazi. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge niwaeleze, tunachofanya tunataka kuwa Taifa lenye uchumi wa kati ifikapo 2025, tuna miaka miwili, tunaweza kuwa tumechelewa, lakini msikate tamaa, your on right truck. Unapokuwa na mashaka na kule uendako umeshaijua njia, haya mashaka mnayoonesha ina maana mmeshaiona njia, kazi mliyoifanya kwa siku mbili imeshanionesha namna gani niendeshe kwa kasi. Nimeona nizungumze hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viwanda vilivyobinafsishwa; kazi niliyopewa moja ni kuhakikisha viwanda vyote bila kujali mmiliki vinafanya kazi vizuri. Viwanda vyote bila kujali mmiliki binafsi na vya Serikali vinafanya kazi vizuri. Ndiyo maana tunazungumza mazingira wezeshi, natambua concern yenu, natambua maelezo yenu katika mazingira wezeshi. Hatuko vizuri kwa muhtasari wa namba, kwamba sisi ni wa 137 kati ya 190, lakini distance to frontier tuko above 50 percent. Sitaki kujivuna na hiyo nitafuata maelekezo yenu na ndiyo maana tunakuja na regulatory reform ya blueprints ambayo hizi taasisi mnazozilalamikia zitalazimika kufanya kazi, inaanza na bajeti mpya kwa sababu ina bajeti implication. Hatukuianza jana kwa sababu ina mambo ya kibajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vilivyobinafsishwa na nimshukuru Shangazi yangu Mheshimiwa Lulida alisema Mwigaje asiwe kondoo wa kafara. Lakini hili la viwanda niko tayari kuwa kafara! Nitahubiri viwanda anayetaka kunipiga risasi anipige risasi, lakini Mheshimwa Lulida unajua mtoto hakui kwa shangazi yake, mimi nilipoelekezwa suala la viwanda, viwanda vilivyobinafsishwa vilikuwa ni 156, tulipokuja kufanya snap shot wakati naambiwa nikiwa Tanga na Mheshimiwa Rais kwamba nimemkwanza, viwanda vilivyokuwa vinafanya kazi vizuri vilikuwa 62, vilivyokuwa havifanyi vizuri tatizo langu vilikuwa 56, vilivyokuwa vina suasua ni 28, vilivyouzwa by stripping (engine peke yake, godown peke yake) vilikuwa kumi. Nikaanza kazi, taarifa niliyowaletea mwezi Machi ndiyo kazi niliyofanya. Katika viwanda 56 troublesome, viwanda 18 vimeshaanza kukarabatiwa na vimekarabatiwa tayari kufanya kazi. Katika kipindi cha mwaka mmoja nawaomba Wabunge mnikubalie muwe na uhakika kwamba nikibaki hapa kufikia mwaka kesho viwanda vinatakuwa vimekwisha vyote. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoja nikuambie viwanda 35 vilivyobaki na nitawasilisha kwa Mheshimwa Spika haya ni mambo ya kitaalam, Waheshimiwa Wabunge viwanda 35 vingine havina sifa ya kuwa viwanda, lakini kwa mamlaka niliyonayo siwezi kuvifuta, inabidi niende kwenye ngazi zinazohusika niwaambie jamani mlichonionesha kama ni viwanda 156 hiki haki-qualify. Mfano, lilikuwepo eneo la kiwanda cha kuunga matrekta, nimeambiwa na kiwanda, nikaenda kufanya survey nikakuta wamejenga shopping mall nzuri kabisa, inaajiri watu inaitwa Quality Center, mimi mall naipenda kwa sababu inazalisha ajira, kumbe tumekosa eneo la matrekta sasa nimetengeza maeneo mengine ya matrekta, ugomvi utoke wapi? Mnanishauri nikabomoe ile shopping mall? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna viwanda vingine vilikuwa vya kupasua mbao, nilipokwenda kuangalia misitu imekwisha, sasa huyo mtu nimfanyeje, nimuue huyo mtu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna viwanda vingine ni mali ya Serikali, kuna eneo kiwanda cha maziwa ni mali ya NHIF, sasa kiwanda cha Serikali siwezi kukichukua nimemwambia NHIF pesa unazo unijengee kiwanda cha madawa, yuko kwenye mchakato ajenge kiwanda cha madawa, ndiyo story za viwanda hivi navimaliza kabla ya asubuhi. Waheshimiwa Wabunge mniamini, wengine wanasema Mwigaje he is not serious, siwezi kujiua! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumze suala la sukari, mimi ni mcha Mungu na mcha Mungu yeyote ni lazima atii na aheshimu dini ya mwezake. Mbali na kuwa mcha Mungu mama yangu ni Muislamu apumzike kwa amani, mama yangu aliitwa Mariamu, nikalelewa na bibi yangu anaitwa Mwamini na Zuhura. Kwa hiyo Uislamu ninao, Mjomba wangu anaitwa Sadiki, kwa hiyo siwezi kuhujumu Uislamu. Mama mdogo wangu mwingine yuko pale, sina tatizo, lakini Watanzania niwaambie tunayo sukari ya kutosha. Tunapozungumza sasa kuna tani 43,000, kwenye stock, lakini Tanzania tunatumia tani 40,000. Bandarini nimeshamwagiza Meneja wa TFDA na TBS sukari iliyoko bandarini inaondoka, ninyi Wabunge ndiyo mnawaonea huruma wale wanaokwenda kufunga na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mbunge yeyote, Mbunge wa kwanza ameshaniambia nimpe tani 1,000 nimemruhusu achukue, njooni mchukue sukari, tuna sukari ya kutosha. (Makofi?Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bandarini tani 22,000 ziko tayari. Mbali na sukari hiyo viwanda vya sukari vyote vimebakiza wiki tatu mpaka wiki nne baada ya dry season vinaanza kuzalisha. Kwa hiyo, asitokee suala la uadimikaji wa sukari ilikuwa ni propaganda na katika propaganda mimi nilisomea propaganda mpaka China ilikuwa ni propaganda sukari ipo, kama ni propagandist mwenyewe ni mimi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kingunge angekuwepo ungemuuliza propaganda alinifundisha Kingunge Ngombale Mwiru. Kwa hiyo, hakuna tatizo la sukari, Wabunge niko hapa na tunafunga kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhani atakayekuwa na tatizo aje aniulize tunasambaza sukari kwenda mikoani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzue suala l sukari nchini, suala hili halikuanza leo na linaenda na mfungo wa Ramadhani, linaendana na rain season viwanda vinapofungwa tumekuwa na haja kama nilivyowafahamisha kwenye sababu tatu za viwanda tulenge viwanda vinavyoajiri watu wengi, kama ilivyo pamba sekta ya sukari inaajiri watu wengi. Sekta ya sukari, kwa mfano kiwanda cha Kagera Sugar kinachozalisha tani 75,000 kinaajiri watu 5,000, lakini Tanzania kama nchi ndiyo wale Wabunge mnasema halafu mnakasirika mnasema shame, wakati mwingine mna haki ya kusema hivyo. Tanzania tuna fursa ya kuweza kuzalisha tani milioni mbili za sukari kwenye mabonde yetu, lakini upaunuaji wa mashamba hayo financiers/wanaotoa fedha walikuwa wanakataa kwa sababu ya uingizaji wa sukari holela na substandard. Tatizo lililompata Kenya, uingizaji wa sukari wa Kenya, sukari wanayozalisha imeshuka kwa 40 percent, sasa tulichoamua Serikali ni kwamba gap sugar tani 135,000 wailete wale wenye viwanda ambao wanalalamika kwamba kuna watu wana- dump sukari halafu wale wenye viwanda tukawapa masharti watuoneshe acreage, eneo watakaloongeza la kuweza kulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niwaeleze kwamba Kiwanda cha Mtibwa wanaongeza, British Food walikuwa hapa kwenye Mei Mosi wakija kutangaza mbele ya Mheshimiwa Rais, wame-commit bilioni 500 Kilombero kuwekeza, pamoja na kuongeza Profesa Jay nikuambie, nitahakikisha maslahi ya wafanyakazi waliopunguzwa wanalipwa pesa zao. Watu wa Mtibwa wanatengeneza bwawa la irrigation 29 square kilometres, Mwenyekiti wa Kamati ni shahidi wameanza system ya irrigation na Kagera vilevile. Mheshimiwa Rais amewapa daraja kuvuka kwenda upande wa Kitengule, tunataka kujitosheleza kwa sukari na ninawahakikishia utaratibu huu ni mzuri, atakayekiuka tunamchukulia hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze alizeti, mawese na karanga ili kuziba lile pengo. Nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Munde Tambwe, amesema kwao Tabora na Wabunge wote wa Tabora na Halmashauri zenu eti mje kwangu niwape trekta, nina matrekta 148, mimi ndiye nawajibika, hizo tractor tatu mlizoomba kila Halmashauri mniletee barua ya Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi

wa Halmashauri, Mkuu wa Mkoa asaini, mlete kwangu kwa mamlaka niliyonayo matrekta zikaanzie kule hamuwezi kutoroka ninyi ni Watanzania. Ngoja tukafanye mazoezi Tabora, Mheshimiwa Munde tukafanye mazoezi Tabora tuta- leverage kwenye Mikoa mingine. Maksudi yake ni nini? Tumeshakubaliana na SAGCOT walete mbegu zenye high yield na ninyi Wabunge najua, kuna Wabunge mnalima alizeti, msilime alizeti ilimradi alizeti, kuna alizeti ambazo ukikamua unapata mafuta mengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, SAGCOT wameshafanya utaratibu, Waziri wa Kilimo ataelezea, tutawapa mbegu lakini ngoja niwaambie na mimi nitakwenda kukamata shamba Tabota nitaanzia Tabora nikikosa Nzega nitakwenda Igunga tulime alizeti, nitahakikisha si mmesema viwanda nivilindwe, nitavilinda viwanda vinavyozalisha mafuta yawe ya pamba, yawe ya alizeti tuondoe hiyo mliyoniambia shame. Nilikuwa naangalia kwenye dictionary, shame ni neno baya mtu akikwambia shame nikamuuliza mwanangu anasema shame maana yake ni nini. Kwa hiyo, nitawahakikishia tunazalisha alizeti na tunapokuwa na alizeti tunaweza kujiokoa na mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze suala la kulinda viwanda, suala la la kulinda viwanda ni wajibu wangu, lakini Watanzania tukubaliane, waliochangia wengine wamehoji utamaduni wa TBS na FCC. Ukienda bandarini haya mambo ya under invoicing na over invoicing kuna nguo zinapita wakishonewa wanafunzi uniform baada ya wiki tatu nguo inakuwa kama chandarua. FCC akizichoma ndiyo hayo maneno ya Mheshimiwa Munira anasema mnachoma nguo za watu, mniongoze nifanye nini. Sasa kwa sababu mmeniruhusu, atakayeleta bidhaa yoyote, TBS nakwambia na FCC wewe choma usisikilize kilio cha huku kwa sababu Waheshimiwa Wabunge wameniruhusu wenyewe. Hiyo ndiyo namna ya kulinda viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, linahusu valuation ya TRA. Suti niliyovaa mimi hii thamani yake ni dola 600, mtu wa TRA akii-value dola 50 unapigwa 25 percent na 18 percent, sasa wewe unataka ipigwe vipi? Mheshimiwa Mpango wametupa ruhusa atakayeleta suti kama hii niliyovaa akasema dola 50 nakuomba tu-uplift kusudi tuipige bei kubwa, tulinde viwanda vya ndani, nadhani ndivyo mlivyonieleza! Ndivyo mlivyotueleza, ndivyo nilivyo waelewa na ndiyo maana viwanda vyetu vinakufa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamezungumza Mwatex, Mwatex ilikufa kwa sababu tulipenda kanga za China ambazo Mheshimiwa Zainabu Mwamwindi anasema akijifunga haiwezi kumfika vizuri, lakini ukiziangalia watoto wa Pwani wanasema zile ndiyo nzuri wanaziita sijui nini zile, ndiyo wanazozipenda sasa tutahakikisha kwamba substandard product tunazi-control, nitalinda viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la tata la Mchuchuma na Liganga. Waheshimiwa Wabunge mradi wa Mchuchuma na Liganga upo, Serikali ilishaaingia makubaliano na mbia kampuni ya China. Kampuni ya China imewekeza pesa karibu dola milioni 60 wamemaliza, wakasaini kitu kinaitwa performance contract, baada ya kusaini performance contract ikabaki kuanza, ndiyo tukaja na sheria yetu ya kuangalia mara mbili tukakubaliana kwamba tupitie ule mkataba tuboreshe vifungu. Wataalam wakaanza kufikia, sasa watalaam kwa maelekezo wao walitumwa kuangalia kama kuna ukakasi au maslahi mapana ya Taifa, ikakutwa kuna vifungu tunavyojadiliana, lakini mwekezaji yuko tayari. Vifungu vya kujadiliana huu ni mkataba wa siri na silazimiki na siyo vizuri kwa wanaojua sheria kuujadili, lakini mimi ni ninyi, ngoja niwaambie mambo mawili na msiwaambie watu. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ule mkataba wa kwanza, ngoja niwaambie, mkataba wa kwanza mwekezaji alikuwa anataka akusanye VAT, aichukue VAT aitumie baada ya miaka 20 atulipe, akasema baada ya miaka 20 niwalipe, sasa ukikutana na watendakazi wa leo wanataka VAT wakatoe elimu bure, wanataka VAT wakanunue madawa wanapata ukakasi. Kwa hiyo, tukakaa nao, kitu kingine na niwashukuru

Wabunge waliochangia chuma cha Mchuchuma na Liganga. Watalaam wa uchambuzi wa migodi wanasema katika ule mgodi deal siyo chuma, kuna madini mengine ambayo kitarakimu yanatija zaidi, wakatuonesha kwa namba na mimi nikawa m dogo kama piriton.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mradi niliupigia kampeni mimi tukamwambia mbia mwenzetu atuletee financial modal, amekwenda kutafuta financial modal ya ku-recognize madini yale na madini haya halafu tutakaa chini na namwambia huyo mbia alipo haraka sana alete financial modal tuanze. Katika utaratibu wangu tukakubaliana kwamba twende tukatengeneze barabara za ndani ramani tunaijua, kiwanda kitawekwa hapa, barabara ya kutokea, mlima uko hapa ndiyo nikaomba pesa ambazo ziko mbele yenu shilingi bilioni tano, lakini kuna shilingi bilioni tano nyingine kama walivyosema, ninakwenda kutathmini upya nijue anayepaswa kustahili kulipwa, kama bilioni moja ndiyo fidia, bilioni nne nitazileta nina Kamati inanisimamia, nina CAG ananisimamia ndiyo Mchuchuma na Liganga, ipo na tutaitumia.

Waheshimiwa Wabunge niwaambie, kuna kitu kinaitwa kulila masimanda, unachukuakitu chako unakiuza, unakuja kwa Kiswahili wanakwambia umeuza kwenye throw price. Kuna nchi moja nilioona kwenye clip walifanya mkataba na wawekezaji, mwekezaji akawaambia we will break even after 30 years, huyu akakubali akasema nipata employment, walipoanza kazi miezi sita aka-break, mwaka wa pili madini yamekwisha, wananchi wakamrudia kiongozi huyo. Nisingependa kuliona hilo na naogopa na nilishawahi kuwaambia sitashiriki kwenye maamuzi yoyote ambayo wajukuu wangu watafunga kaburi langu minyororo, ndiyo hiyo Mchuchuma na Liganga, mniamini, niko serious, watu wengine wanasema Mwijage hayuko serious, hivi sura hii iwe serious itafananaje, mtaiangalia? I am serious (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze suala lililozungumzwa sana la mkakati wa pamba mpaka mavazi.

Nimewaita wenye viwanda vya nguo, wenye ginneries nimekaa nao watu wenyewe wa kwenye field, wameeleza maeneo wameeleza maeneo ambayo yana ukakasi, nilikuwa na watu wa Wizara ya Fedha tunayashughulikia, lakini Mheshimiwa Waziri wa Nishati amezungumza, tunapeleka umeme. Kwa hiyo, tunathamini cotton to clothing kama mlivyosema siwezi kusema tena, ndiyo sekta yenye ajira nyingi. Kwa mfano, Kanda ya Ziwa nimeeleza kwenye speech yangu kwamba Social Security Funds wamekwenda kufufua ginneries, tunapambana zinunuliwe zaidi lakini kuna ginneries za sekta binafsi, muulize Mheshimiwa Kishimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua kuna watu wengine anamiliki lakini hataki kujulikana anamiliki, Kishimba anamiliki na anasema anamiliki. Sasa kuna ginneries za Tanzania, uzoefu tulio nao hakuna ginnery ilikuwa inaweza kufanyakazi kwa siku 90, sasa pamba imezalishwa kwa wingi, tunakwenda kuiunganisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kuzungumza kidogo kwa heshima na taadhima, watu waliosema The Government is not coordinated, No! tuko coordinated. Mfano, ni cotton to clothing, ilipopigwa baragumu ya pamba mpaka mavazi, Waziri Mkuu alikuwa Kiranja wetu Mkuu, alikuwepo Charles John Tizeba, Waziri wa Kilimo, alikuwepo Waziri wa TAMISEMI, Jafo tukakimbia wote na Mheshimiwa Selemani Jafo, tukaanza kuzunguka nchi nzima, ndiyo matokeo haya tukisaidiwa na ma-DC, tukigawa kamba, tukapanda, Mungu atatusaidia pamba itavunwa nyingi, lakini tutavilinda viwanda vilivyopo ili viweze kuchakata pamba yetu. Ndiyo nataka kujibu hilo kwamba mniamini. Cotton to clothing tunaijua na nimezungumza kwenye mikakati midogo kwamba na yenyewe ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaeleze Waheshimiwa Wabunge, kuna Mbunge mmoja kazungumza vizuri kwamba haya mambo yanabadilika, yatakapobadilika wote tupo Tanzania mnieleze. Mimi napatikana, kwa simu napatikana, hata kwenye kahawa nakuwepo tuzungumze. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la kukwamisha Wawekezaji na nizungumze kesi ya Hanang’. Mimi ndiye niliyepewa dhamana na nitahukumiwa kwa kutoakuanzisha viwanda. Kama nilivyowaambia, kufufua viwanda vilivyokufa na vile vilivyopo kuzalisha ukomo lakini kuanzisha vipya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mamlaka niliyonayo nitamtuma Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda aende Hanang amtafute yule mwekezaji aliyetaka kutengeneza kiwanda cha saruji nije nisikie mtu anayekataa nitampandia juu, nitampandia juu kwenye mamlaka iliyotuteua! Haiwezekani, huwezi kuchelewesha mwekezaji. Mbunge wa Hanang usiwe na wasiwasi, kiwanda cha saruji tunakihitaji, atakayetaka kujenga kiwanda afanye utafiti na utafiti utafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo TIRDO, nimewaambia ndugu zangu, ukitka kuenga kiwanda kama wewe ni mwenzangu nenda SIDO, kama inafikiri una ubavu nenda TIRDO. Hata uki-hire consultancy, niwaambie tahadhari enyi wawekezaji na Wabunge muwe wawekezaji na niwashukuru wale Wabunge ambao mnakuja kuwekeza na mnaanza kujenga, mnaniletea picha kwa whatsapp, msiniletee picha mnialike mimi nina gari nzuri, nitakuja nifungue viwanda hivyo. Tunadanganyana, kuna watu wanafungua viwanda vidogo, wanapata tija halafu wewe unabaki viwanda vidogo mimi sivitaki, wenzako wanakula ,wewe unasusa. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la mazingira ya biashara. Nawashukuru mlinishauri vizuri, lakini siyo kwamba nchi hii siyo ya uwekezaji. Ninawaahidi nitaboresha zaidi, regulatory reform ikija mtaona mambo yanakuwa mazuri, mambo yatakuwa mazuri.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Lucy Mayenga uliyozungumza yote kuhusu mazingira ya biashara, najua watoto tunawazaa wenyewe. Mimi mtoto wangu anaweza akapata kazi Fair Competition au TBS akikosea siyo mimi. Sasa kama nilivyowaeleza, Mheshimiwa Lucy Mayenga yote mnayoyaona mje mtuambie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, brother umezungumza mambo ya ukaguzi wa bidhaa kule Dubai, njoo uniambie, umekuwa kwenye Wizara hii ukisimami sekta hii unaijua vizuri njoo uniambie. Mabadiliko unayoyasema kama SGS anaongeza gharama nitayatekeleza. Sina maslahi binafsi mtu kukwamisha wawekezaji. Kwanza wawekezaji wanapokuja wengi ujiko unakuja kwangu, mnasema Mwijage umejenga viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze suala la kujenga viwanda. Serikali haijengi viwanda ila inaweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi kuwekeza. Tuko vizuri, soma hotuba yangu nimeeleza nafasi yangu na Tanzania Private Sector Foundation, muulize Mzee Mengi.

Nimezungumza na Mzee Mengi wakati nahamasisha viwanda vya madawa ilikuwa juzi tu tumeweka jiwe la msingi kiwanda chake. Tunazungumza na biashara ni kuzungumza kama mikono miwili ilivyo, mikono miwili ni kunawishana, kwa hiyo hatuna tatizo na private sector. Hii migongano iliyopo mtu anapopata matatizo aje atueleze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Chumi alizungumza suala la mifuko. Hilo suala la mifuko ya plastic ni suala la kiutawala. Katibu Mkuu wangu usimame, angalia hiyo mifuko inakwendaje na uanze utekelezaji bila kuchelewa.

Tumezungumza suala la fidia za EPZA, Mheshimiwa Kawambwa, Kaka yangu twende tukae chini, tuangalie Bagamoyo tutakavyoweza kuiweka vizuri na niwaeleze kuna watu waliandika wakihoji kuhusu Bagamoyo Special Economic Zone. Bagamoyo Special Economic Zone ninavyozungumza sasa mwekezaji yuko Dar es Salaam na timu ya Serikali wanajadiliana. Upande wa viwanda wamemaliza, sasa wanajadiliana upande wa bandari ndiyo taarifa niliyonayo, mambo yanakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuko mwaka wa pili katika safari ya miaka kumi ya kufika uchumi wa kati. Watu wangependa kufika leo lakini naona muende taratibu tutafika lakini muendelee kunielekeza na kunikosoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la Mheshimiwa Mariam Kisangi. Tumekubaliana na Meneja wa TanTrade kwamba siku za sikukuu wenye biashara mtaingia kuuza bila kujali kama ni Sabasaba au siyo Sabasaba wale wananchi wa Dar es Salaam na watoto wataingia bure. Mheshimiwa Mariam Kisangi amependekeza bembea, sasa tunatafuta nani aweke bembea na atafute mtu binafsi aweke mabembea mtoto kipanda weka shilingi 50, msiwa-charge pesa nyingi, mkitaka profit nitawafukuza, watoto waende kuburudika na watoto hawana pesa au wacheze bure kwa sababu hawana pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Benardetha Mushashu umezungumzia suala la viwanda Kagera, namsubiri Waziri wa Mifugo, tumepata mwekezaji ambaye atatengeneza kiwanda cha maziwa, shamba la kutengeneza maziwa kuanzia maziwa kwenda kwenye UHT mpaka maziwa unga. Mheshimiwa Lwakatare anasema Mwijage usikimbie ukapita kwenu. Bibi yangu aliyenilea, alinimbia Mwijage ukiamka unawe uso na uso ni Jimbo langu, uso ni nyumbani, lakini mimi najenga Tanzania. Kwa hiyo, usiwe na wasiwasi Mama Mushashu nitakuja kuwaelekeza namna gani ya kujenga viwanda. Wewe shangazi yangu unielewe, usiogope kuanza na kiwanda kidogo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la kiwanda kidogo sana nilizungumze, mwenzangu mimi hujawahi kumiliki hata milioni moja, unakwenda kutafuta bilioni 100 utaanguka nayo, anza kidogo. Siri ya kiwanda kidogo maana yake ni nini? Tunataka kurithisha utamaduni wa kumiliki biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie hili, tunataka kujenga utamaduni wa kupenda viwanda. Nimetoa mfano huu siyo wa kibaguzi. Wenzetu Wahindi na Waarabu watoto wao tunasoma nao, lakini kwenye kazi hatuombi na wao. Nilikwenda Manyara kwenye kiwanda cha sukari, nimekuta watu mle wana historia ya viwanda, wameanza kwenye kiwanda kile cha sukari mpaka kinakua, mtoto na watoto wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kueleza maelezo hayo nitayafafanua zaidi nikipata nafasi, naomba kutoa hoja.