Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Bismillah Rahman Rahim. Nataka kumshauri tena Mheshimiwa Waziri na naomba anisikilize vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1979 nikiwa na umri wa miaka 14, nilifika katika uwanja wa mapambano ambapo wanajeshi wetu walipambana na majeshi ya Iddi Amin. Miaka 40, mwaka huu mwezi Machi, nilifika tena katika maeneo yale, nikamwomba Mwenyekiti wangu tutembelee maeneo ya makaburi kule Kaboya. Nikatembea na Kamati. Tulitoka Kaboya, baada ya kumaliza mpaka barabarani, hakuna mtu anaongea na mwenzake ndani ya gari. Sasa asiyejua kufa, aangalie kaburi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, anaposema kwamba kuna usalama ndani ya mipaka yetu, sikubaliani naye unless yeye na Jeshi lake na makamanda wake, wanipe tafsiri ya usalama ni nini? Maana labda kufa mtu mmoja mpaka 54 kwao bado ni amani. Mimi sikubaliani kabisa kama kuna amani. Haiwezekani Mtanzania afe ndani ya ardhi yake kwa sababu ya mali yake, halafu watuambie kuna amani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Waziri wa Maliasili. Kama mimi ndio ningekuwa Waziri siku ile, ningetoa kauli mbaya zaidi kuliko ile. Haiwezekani Watanzania wenzetu wanauliwa ndani ya ardhi yao kwa mali yao halafu tunasema tuna amani. Kwa sababu gani? Mimi sikubaliani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, anapaswa ajipange, hii ndiyo nchi. Hii Wizara anayoiongoza yeye hii ndiyo nchi, jeshi ndiyo nchi, haya maringo na kujidai kwetu ni kwa sababu ya hawa. Sasa bila hawa, hatuna amani, hatuwezi kuwa na nchi. Sikubaliani kabisa na Mheshimiwa Waziri na namwomba sana, hawa makamanda, miaka 40 hiyo iliyopita, mimi nimeenda kule wengine hawakuwa Wanajeshi na wengine ndiyo wanaanza Jeshi. Awapeleke kule wakaone yale makaburi, ndiyo watajua jeshi ni nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna matatizo kwenye mipaka yetu. Namwomba Mheshimiwa Waziri na Wizara, wadau wenzake, zile barabara, kilometa 54 za mpakani, ile barabara ijengwe ili Wanajeshi wetu na Kamati ya Ulinzi na Usalama katika Wilaya ile ya Misenyi iweze kufanya patrol ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Waziri, akae na Wizara zote, kama ni Ardhi, Miundombinu na kadhalika, wajenge ile barabara. Tumekwenda kule, huwezi kufika. Sasa likitokea lolote, wanajeshi wetu watakufa, hawajapata usaidizi. Haiwezekani, hakuna amani. Namwambia Mheshimiwa Waziri, hakuna amani, lakini kwa sababu ya muda, sitasema sana, ningechambua sana hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, bajeti iliyopita nilimwonesha vyanzo vya fedha nikamwambia UN Mission ni fedha. Kuna nchi kama Bangladesh zinaendesha nchi zao kwa UN Mission tu. Mheshimiwa Waziri, anunue vifaa. Kila kifaa kinalipwa katika UN Mission. Tuna Wanajeshi wetu katika UN Mission, kwa nini tunakosa fedha za kuendesha Jeshi? Haiwezekani. Hilo moja la mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile vifaa hakuna. Wanajeshi wetu walioko katika vita hawana vifaa. Ushahidi ni huu wa DRC. Haiwezekani Wanajeshi wetu wavamiwe, ndani ya masaa 13, wanapigana hakuna mawasiliano, hakuna rescue. Thirteen hours Wanajeshi wanapambana mpaka wanaishiwa risasi, wanakuja kufa, ni uzembe. Inauma kweli kweli! Sisi ambao tumeshuhudia maeneo yale ya vita, inatuuma. Mtanzania mmoja kufa, inatuuma! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani, ule ni uzembe. Mheshimiwa Waziri akituambia kwamba sijui walivamiwa, mimi sikubali, najua ni uzembe. 13 hours Askari wa kulinda amani anapigana, ana silaha ya kawaida tu, ana risasi 90. Anapigana kwa uadilifu, wamejipanga kwa sababu ni weledi, 13 hours, hakuna rescue, halafu Mheshimiwa Waziri anatuambia nini hapa? Sikubaliani na hili, Mheshimiwa Waziri, anunue vifaa, Wanajeshi wetu waende wafanye kazi kwa uangalifu, lakini pia ni faida vile vile kwa Taifa. Hivyo, Mheshimiwa Waziri anunue vifaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo nataka niliseme na hili tutakuja kupambana sana kwenye mshahara wa Mheshimiwa Waziri. Nilisema Wanajeshi hawa, wapatiwe angalau bima basi. Haiwezekani, mwanajeshi anastaafu anadhalilika, anasawajika.