Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Wizara hii, japo nimechangia kwa maandishi na haya mengine machache niwasilishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala ambalo nataka nianze nalo ni hili suala la Wanajeshi wanavyokwenda kwenye mafunzo yao mbalimbali lakini kuna zile stahiki zao wanakuwa wanapewa zile pesa za chakula laki tatu. Sasa wakienda kule zile posho zao wanakatwa elfu nane, ukizijumlisha zinakuwa laki mbili na arobaini. Kwenye familia labda ameacha labda elfu sitini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza hivi vyanzo vya mapato vinaongezwa vipi kwa sababu ukiangalia hizi stahiki zimekuwa ndogo sana na hapo naomba pia Mheshimiwa Waziri atakavyokuja kuhitimsiha hapo aseme hii stahiki aichambue kwa sababu haijakaa vizuri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusu Kikosi cha Upelelezi cha Jeshi. Naomba kwa sababu sasa hivi kwa kweli Tanzania tumeingia katika taswira mbaya kwa sababu Waasisi wa Taifa hili walitujenga vizuri sana, sasa kuna matukio ambayo yanatokea hata hatujui yanatoka wapi. Kwa hiyo, haya matukio yamekuwa yanachafua Tanzania. Hawa watu wasiojulikana, hawa watu unakuta sasa wanadhuru hata raia wasiokuwa na hatia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kutumia chombo cha Upelelezi cha Jeshi la Wananchi wasaidie Polisi, ili angalau sasa hawa wanaochafua Tanzania, hilo genge la wahuni linalojihusisha na haya mambo lidhibitiwe. Kwa sababu najua Vyombo vya Ulinzi na Usalama kila kikosi kina Wakuu wake wa kuripoti taarifa na matukio mbalimbali. Sasa naona kama Polisi kidogo wanayumba, niombe sana Jeshi la Wananchi hasa Kikosi cha Upelelezi washirikiane na Polisi kukomesha haya matukio. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija kwenye SUMA JKT, kwa kweli wanajitahidi. Tuangalie ni namna gani sasa hata vitu ambavyo vinaongezea mapato, tuangalie tu hivi vya Bunge tulivyokalia havina ubora wowote, vimetengenezwa kwa muda mfupi na vimeharibika kwa muda mfupi. Kwa hiyo, sasa niombe hata kama kuna marekebisho ambayo yanataka kuja kufanyiwa kwenye hivi viti wapewe SUMA JKT ili nao zile pesa zibaki huku SUMA JKT na jeshi nalo wapate mapato kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu pia kuna manung’uniko na Mheshimiwa Waziri pia atakuja kusema hapa, kuna pesa zinakatwakatwa sijui shilingi elfu kumi za kuchangia umeme, kama hili jambo ni la kweli hebu aje atuambie kama kweli kuna Wanajeshi wanakatwa. Kwa sababu ukiangalia Jeshi kwa sasa hivi walikuwa wanategemea angalau yale maduka kama alivyochangia Mbunge mwenzangu, walikuwa wanapata angalau kwenda kukopa na kujikimu kwa sababu masaa 24 wapo kazini. Ukiangalia hawana kipato chochote lakini sasa ukiona kama kuna vipesa ambavyo labda vinakatwa vya kuchangia umeme, hilo kwa kweli naomba Mheshimiwa Waziri aje alitolee ufafanuzi ili tuangalie sasa ni namna gani ya kuboresha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni tatizo, tunakaa hapa tunapitisha pesa sasa zile pesa tukishapitisha bajeti, bajeti haiendi kwa wakati muafaka na ukiangalia hapa wanasema hakuna mahali popote Afande anaweza kwenda kulalamika. Kwa hiyo, tumwombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha pesa inayotengwa ya Jeshi la Wananchi ipelekwe kwa wakati muafaka ili nao sasa wapate kutatua kero zao na mahitaji yao waweze kupata huduma zao za Kijeshi pamoja na familia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wale Askari wanaohamishwa na wanaostaafu pia nao wapewe stahiki zao. Unakuta hata zile pensheni zao ni ndogo sana, tuangalie sasa ni namna gani Serikali angalau iwaongezee zile pensheni zao, wale ambao pia wamepandishwa vyeo tuangalie ni namna gani ya kuwaongezea marupurupu katika vyeo vyao, siyo kuwavalisha tu nyota lakini zile nyota ziendane na stahiki zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu makazi. Makazi hata zile nyumba ambazo zimejengwa na Serikali lakini bado ni mbovu zinatakiwa matengenezo. Sasa bado kuna changamoto kubwa sana, Wanajeshi wengi wanakaa uraiani, niliwahi kusema hapa nikasema kuna watu wanatumia mwamvuli wa Jeshi la Wananchi kuvaa sare za Jeshi la Wananchi wanafanya uhalifu lakini siyo Jeshi la Wananchi. Kwa hiyo, naomba tufanye upelelezi hizi sare kama kuna watu wanaotengeneza hizi sare wachukuliwe hatua na nidhamu za kisheria.