Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa hotuba nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimboni kwangu Buhigwe, Wilaya ya Buhigwe, tunao wanajeshi wanaolinda mipaka vizuri lakini hawana vitendea kazi kama magari na pikipiki. Ombi langu ni kupatiwa vitendea kazi na kwamba makazi hafifu viboreshwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uniform za wanamgambo tunaomba ziboreshwe kwani ni walinzi imara katika maeneo yetu, wengi hawana uniform na taratibu ya namna ya kuzipata hawaelewi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Wizara ya Nishati katika mapato watenge fedha za ukarabati wa ukuta wa Mererani kwa mwaka ujao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza tena Mheshimiwa Waziri kwa kusimamia Wizara hii vizuri. Nawapongeza pia kwa kumpandisha cheo Mkuu wangu wa Wilaya ya Buhigwe.