Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze mchango wangu kwa kumwomba na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia uhai na afya na kuniwezesha kutoa mchango wangu kwenye Wizara hii. Katika Wizara hii nitakuwa na mambo makuu matatu au manne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na migogoro ya ardhi kati ya maeneo ya majeshi na wananchi, yako maeneo mengi, aidha wananchi wamevamia maeneo ya jeshi au wanajeshi wamevamia maeneo ya wananchi. Kwa mfano katika Wilaya ya Nachingwea, ni vizuri sasa mgogoro huu ukaisha kabla haujaleta madhara makubwa. Katika kukabiliana na mambo haya ni vyema sasa maeneo yote ya Majeshi yakapimwa ili kuwapatia Hati Miliki na hivyo kutambulika rasmi kwa mujibu wa sheria. Maeneo ya Jeshi kukosa hati miliki ni jambo baya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kuishauri Serikali ni kuikamilisha bajeti ya Wizara hii, kwa maana ya fedha za miradi ya maendeleo. Kuacha kutoa fedha za maendeleo katika Wizara hii ni kudhoofisha ulinzi na usalama wa nchi yetu. Kwani hakuna ulinzi endelevu bila ya miradi ya maendeleo hasa kuwa na vifaa vya kisasa na kuendelea kuwa na mafunzo ya mara kwa mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kusikitisha sana kuona wanajeshi wetu hawana Bima ya Afya zao pamoja na kuwa na Hospitali za Jeshi. Bima ya afya kwa wanajeshi na familia zao ni muhimu sana, kwani wako wanajeshi ambao wanaishi nje ya Kambi za Jeshi hivyo, wanapopata matatizo ya usiku wanakuwa mbali na Hospitali za Jeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu malipo ya wastaafu kuchelewa ni jambo la hatari sana kwani wanajeshi hao wameitumikia nchi yetu kwa weledi mkubwa na hivyo kuchelewa kuwalipa ni kutowatendea haki zao. Naishauri Serikali kutoa fedha zote zilizopitishwa na Bunge na zitoke kwa wakati ikiwa na mafao ya wafiwa ambao familia zao zimepoteza wapendwa wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi Kushiriki Shughuli za Kisiasa. Kumeanza kuibuka utamaduni wa kushirikisha wanajeshi kushiriki kwenye shughuli za kisiasa. Jambo hili linaweza kupunguza sifa nzuri ya Jeshi letu, jambo hili ndilo linaloharibu Jeshi la Polisi kwani Jeshi la Polisi huwezi kulitenga na siasa kwani ni jambo la kawaida sana nchini kuona Polisi wakifanya siasa hadharani. Naishauri Serikali kuacha mara moja tabia hii isije ikatuletea madhara makubwa nchini. Wanajeshi waachwe wakae makambini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Jeshi linaloitwa Jeshi la Akiba (Mgambo). Jeshi hili hivi sasa halijapewa kipaumbele kama mwanzo kuanzia bajeti yake mpaka watumishi walioko kwenye halmashauri zetu Makamanda wa Mgambo wa Wilaya na Mikoa hawana vitendea kazi muhimu na fedha za kutosha kuendesha ofisi zao. Maafisa hawa huonekana wakati wa kuandikisha wanamgambo wapya tu na wakati wa kuandikisha vijana wa kwenda JKT. Vile vile vyeti vya vijana wanaomaliza mafunzo ya Jeshi la Akiba (Mgambo) vinachelewa sana na pengine kukosekana kabisa.