Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

shukrani kwa utaratibu huu mzuri ambao unatuwezesha kutoa mchango wetu kwa wale ambao hatujapata nafasi ya kuongea.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Waziri na Naibu Waziri pamoja na watendaji wote wa Wizara hii kubwa na ambayo ndiyo uti wa mgongo wa maendeleo na ukuzaji uchumi kwa Taifa letu hasa kwa wananchi walio wengi. Wizara hii ndiyo pekee itakayomwondolea umaskini mkulima, mvuvi na mfugaji pamoja na wote wanaotegemea mazao yatokanayo na sekta hizi. Naomba nitoe maoni yangu kama ifuatavyo:-
(i) Ukitaka mali utaipata shambani:-
(a) Endapo Waziri utawapatia nyenzo za kisasa wakulima wako kama trekta, power tiller, jembe la ng‟ombe na kadhalika;
(b) Mbolea, pembejeo za aina zote ambazo zitamfikia mkulima kwa wakati na za kutosheleza; na
(c) Maafisa Kilimo wapelekwe vijijini kuliko na wakulima ili watoe ushauri wa kitaalam.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na ushauri huo, naomba Mkoa wa Singida uingizwe kwenye orodha ya mikoa inayolima mahindi kama zao la biashara ili kuweza kuwapatia pembejeo (mbegu) ya zao hili. Zao la vitunguu katika Mkoa wa Singida lipewe kiapumbele kama ni zao la biashara, pia na kupewa pembejeo. Zao la alizeti, bado wakulima wengi wanalima kwa mkono, hivyo, tunaomba trekta angalau kila Kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kuhusu matrekta ya SUMA JKT ambayo yalisaidia sana na ndiyo yaliyoinua ongezeko la kilimo kwa mazao yote, kwani yalikuwa yanatolewa kwa mkopo wa Halmashauri zilikuwa zinawadhamini wakulima na utaratibu huo uliwasaidia sana. Je, ni kwa nini SUMA JKT hawana tena utaratibu huo ambapo walishirikiana na TIB au Benki ya Kilimo?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishie hapo. Ombi langu ni:-
(i) Pembejeo ya zao la mahindi Singida;
(ii) Zana za kisasa za kilimo;
(iii) SUMA JKT warejeshe utaratibu wao wa kukopesha matrekta kwa kushirikiana na TIB kupitia Wizara ya Kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.