Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa uchapa kazi wake. Hata hivyo, nina mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, J.K.T. Hivi karibuni ilianzishwa kwenye eneo la shamba la Milundikwa la zamani ambapo shamba hili lilipomaliza/sitisha kazi zake eneo hilo lilitumiwa na JKT na baadaye Serikali iliamua kuwarudishia wananchi ambao hapo kabla eneo lilikuwa mali yao. Shamba lina ekari 27,000 na katika kurudisha kwa wananchi vilipewa vijiji vya Milundikwa ekari 12,000, Kasu ekari 2,000, Kisura ekari 2,000 na Malongwe ekari 1,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ekari zaidi ya 7,000 ziliachwa kwa Halmashauri ya Wilaya kwa maelekezo ya kupanda miti na utunzaji wa mazingira. Wananchi wameendelea kutumia ardhi hiyo toka mwaka 1998 hadi mwaka jana 2017 ambapo wameondolewa; na zaidi ya watu 4,000 hawana mahali pa kulima na kuna mali zao mbalimbali kama miti, nyumba na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali isichukue eneo lote, wachukue ekari 7,000 ili wananchi waendelee kulima maeneo waliyopewa na Serikali na ieleweke si wavamizi bali walipewa. Tunahitaji uwepo wa Jeshi lakini tunaomba tusaidiwe eneo la kulima. Eneo lote halitumiki, limekaa bila matumizi hata kama patakuwepo matumizi. Naomba Serikali ipokee ombi letu na kulitafakari kwa manufaa ya ustawi wa jamii yetu kiuchumi na kijamii pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi pia iendeleze mila na desturi yake ya kukaa na jamii kwa amani ili kuwawezesha wananchi kunufaika na uwepo wake, kuiga matumizi ya sayansi na teknolojia mbalimbali ikiwemo kilimo, biashara, michezo na mchango wao wanaoutoa kutatua tatizo la upungufu wa walimu kwenye Sekondari ya Milundikwai na wafanye hivyo hata kwenye zahanati zetu za vijiji vinavyozunguka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.