Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Watendaji wa Wizara kwa kazi kubwa na nzuri wanayofanya kwa Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi kubwa inayofanywa na Wizara hii, bajeti ambayo huwa inapangwa na kuidhinishwa inatolewa kidogo, hata hiyo kidogo haipelekwi kwa wakati. Ucheleweshwaji huu unaathiri utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Fungu 38 lilipokea asilimia 41 tu ya fedha ambazo zilitengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niipongeze kazi nzuri inayofanywa na SUMA JKT. Naomba Serikali kuboresha maslahi ya walinzi wa SUMA JKT Guard. Pesa inayolipwa kwa walinzi hawa haiendani kabisa na living cost za sasa. Taifa tunaendelea kuwa na amani na usalama kwa sababu Jeshi letu linafanya kazi kubwa usiku na mchana, lakini hali ya kimaisha/living conditions zao ni mbaya sana. Nyumba za kuishi bado haziridhishi. Kama Taifa tuna wajibu wa kuhakikisha wana makazi bora (Makambi) na siyo waachiwe kuishi mitaani ambapo tumejionea baadhi yao wamekuwa wakijihusisha kwenye vitendo visivyopendeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa kuwa tax exemption kwenye yale maduka ilifutwa, basi Mheshimiwa Waziri atueleze Jeshi wameongezewa allowances kwa ajili ya manunuzi ya mahitaji muhimu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa na ukusanyaji kwenye ukusanyaji wa madeni kwa wale waliokopa matrekta, ushauri wangu kwa Serikali tutumie list of shame bila kujali nafasi ya watu hata kama ni viongozi wa juu. Nadhani hii itashawishi watu kulipa madeni yao kwa kupitia magazeti na televisheni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.