Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kutoa mchango wangu katika hoja ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetusaidia afya na uzima tumefika jioni hii ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo, nichukue nafasi hii kumpongeza Ndugu yangu Mheshimiwa Waziri Hussein Ally Mwinyi kwa kazi yake nzuri na ya kizalendo anayoifanya katika Taifa hili. Pia niwapongeze wakuu wetu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kazi yao nzuri ya kulinda mipaka yetu pamoja na wataalam wote wa Wizara kwa utendaji wao mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kutenga fedha katika bajeti hii kwa utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami toka Ubena Zomozi mpaka Kizuka Ngerengere kwenye kiwanja chetu cha ndege na barabara tunayoitumia kufika Ngerengere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ujenzi wa barabara hii lakini nina maombi mawili. Ombi langu la kwanza ni kuiomba Serikali kujenga barabara hii toka Ubena Zomozi mpaka Ngerengere Mjini ili kipande kile cha kilomita kilichobaki pia kijengwe kwa kiwango cha lami ili kupeleka maendeleo kwa wananchi wa Tarafa nzima ya Ngerengere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu la pili ni kwa kuwa tuna Kambi nyingine ya Sangasanga ambayo inatumia barabara ya Mdaula mpaka Sangasanga. Nichukue nafasi hii kuomba Serikali pia kutengeneza barabara hii toka Mdaula - Sangasanga mpaka Ngerengere Mjini kwa kiwango cha lami ili kuunganisha barabara toka Ubena Zomozi - Kizuka - Ngerengere na Ngerengere - Sangasanga - Mdaula na kurahisha mawasiliano ya kambi zetu za Jeshi toka katika uwanja wa kijeshi lakini pia kuimarisha mawasiliano na mwingiliano wa wananchi wetu kwa urahisi na kuboresha maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, nina ombi kwa Jeshi Kambi ya Kinonko kuhusu mgogoro wa ardhi kati ya kambi na wananchi wa Kijiji cha Sinyaulime, Kitongoji cha Kipera ambapo wananchi walikuwa pale kabla ya Jeshi kuhamia pale. Naomba Jeshi liwaachie wananchi maeneo haya sababu wanatayategemea kwa makazi na kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.