Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze na mifugo. Hoja kutoka Mkoa wa Simiyu, kwanza kwa kutozwa ushuru mara mbili aidha wauze au wasiuze, analipa ushuru shilingi 6,000/= ilhali wanaopelekea ng‟ombe Mnadani sio wote ni wafanyabiashara, bali wanapeleka ili wauze wapate mahitaji yao kama vile kununua chakula cha familia zao. Sasa unapomwambia auze au asiuze huu ni uonevu wa hali ya juu sana. Kwa maana nyingine ni wizi. Naomba Halmashauri ya Bariadi Mjini itazamwe katika hili na Mnada wa Dutwa Bariadi Vijijini kwani ni tatizo kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata Waziri Mkuu alipokuja kwenye ziara yake Mkoa wa Simiyu alikutana na kero hii na alitoa ufafanuzi kwenye mkutano wa hadhara akisema mauzo yanafanyika mara tu biashara inapokuwa imefanyika. Alisema ni marufuku mwananchi kutozwa ushuru mara mbili, lakini kauli yake imepuuzwa, kwani bado wananchi wanaendelea kutozwa kila kichwa ng‟ombe sh. 6,000/= auze au asiuze, analipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, majosho mengi ya kuoshea mifugo yalishakufa kutokana na kukosekana fedha za kuendeleza majosho kutokana na ufisadi. Wananchi wa Maswa Meatu baadhi yao hawana mahali na kuchungia mifugo yao. Naomba Serikali irudishe pori la Maswa, lirejeshwe kwao ili liwasaidie kuondoa mgogoro wa wakulima na wafugaji, kwa sababu pori hilo limekosa sifa ya kuwa Hifadhi ya Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mkoa wa Simiyu, wananchi wa Simiyu wengi wao ni wakulima wa pamba; wamekata tamaa kulima zao hili kutokana kuuzwa kwa bei ya hasara. Kwa muda mrefu hivyo wamekata tamaa na badala yake kulima zao la choroko kama sehemu ya zao la biashara. Kwa hiyo, naomba Serikali ilitazame kwa umakini zaidi kwani zao hilo limepotea kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Serikali irudishe mbegu za pamba ambazo zilikuwa zinatumiwa zamani, zile zenye manyoya, kwani hizi nazo hazioti kabisa. Serikali ipandishe bei ya pamba badala ya kununua pamba kwa sh. 650/= mpaka sh. 750/= iuzwe sh. 1,500/=. Kwani mbona soda ambayo akina Mengi wanakologa maji na kuweka sukari wanafunika, lakini wanauza sh. 1,000/=? Iweje wananchi ambao ameiandaa pamba yake kwa muda wa miezi sita mpaka saba anauza sh. 650/=. Naomba zao hili liangaliwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, njaa Mkoa wa Simiyu haikuwepo kwa miaka mingi sana, lakini Mkoa wa Simiyu kwa sasa unaongoza kwa janga la njaa. Hiyo ni kutokana na wananchi hawa kulima na baadaye kuuza mazao yao kwa hasara kabla ya wakati, baadaye kujikuta hawana chakula. Hivyo ,naomba Serikali iwape elimu kuhusu utunzaji wa chakula chao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mageti ya mazao kila kona na bila hata ya utaratibu maalum. Mageti haya yamesababisha vifo; nashauri wayawekee taa, kama hawawezi kuweka taa na hawalindi usiku, basi wayatoe kwa wakati wa jioni wayarejeshe asubuhi, kwani ni hatari sana. Serikali itoe maelekezo kwa Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha mchango wangu.