Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Katibu Mkuu, Mkuu wa Majeshi na timu yote chini ya Wizara hii kwa utendaji wao mahiri na makini ndani ya Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua umuhimu wa Wizara hii, tatizo ninaloliona ni kuwa tunapitisha bajeti lakini mwisho wa mwaka hawapelekewi fedha zote. Wizara hii ina mambo mengi muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu. Hivyo lazima Hazina waone umuhimu wa kuwapelekea fedha zote za bajeti tunazopitisha. Nasema hivi kwani binafsi nilikuwa kwenye Kamati hii ya Ulinzi na Usalama (KUU).

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulitembelea eneo la karakana ya JWTZ iliyoko Kibaha, tatizo kubwa ni uchakavu wa mitambo ya kijeshi ndani ya nchi yetu. Tunatambua kwa kuboresha karakana hizi, ikizingatiwa kazi kubwa ya jeshi letu ni kulinda mipaka ya nchi zetu, amani tuliyonayo italindwa kwa asilimia kubwa na Jeshi letu au majeshi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba mafunzo ya JKT kwa vijana wetu yaongezwe hususani kwa wale waliomaliza Kidato cha Sita, ambao hawakupata nafasi ya kujiunga na hivyo kumaliza Chuo Kikuu bila kupata mafunzo haya ya JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, nashauri Bajeti ya JKT iheshimiwe na kupelekwa yote na ikiwezekana kila mwaka bajeti iongezwe ili kutoa fursa kwa vijana wengi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niendelee kumpongeza Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.