Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru nami kwa kupata nafasi ya kuweza kuchangia katika sekta muhimu katika nchi yetu, lakini pia na duniani kwa ujumla. Napenda kusema kwamba sekta ya kilimo ni sekta ambayo inazalisha mara 11 zaidi ya sekta nyingine katika nchi za Afrika hususani zilizopo katika Ukanda wa Jangwa la Sahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kuzungumzia vyama vya ushirika. Kumekuwa kuna migogoro mingi sana kwenye Vyama vya Ushirika. Vyama hivi vimeanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika ya Mwaka 2013 na mwenye mamlaka ya kushughulikia na kusimamia migogoro yoyote ndani ya Vyama vya Ushirika ni Ofisi ya Mrajisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakuu wetu wa Mikoa na Wilaya na viongozi wengine wamekuwa wana-interfere sana sekta hii ya Vyama vya Ushirika na hivyo kusababisha matatizo. Wamekuwa wana-interfere katika suala zima la masoko, lakini pia katika suala zima la uchaguzi, kwamba nani awe kiongozi wa ushirika? Wamekuwa na interference kubwa sana, kitu ambacho kinatuletea migogoro na vyama vyetu vya ushirika vinashindwa kujiendesha kama vyama binafsi na hivyo vinaonekana kama ni vyama ambavyo vinaingiliwa na siasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumwambia Mheshimiwa Waziri kwamba wananchi wa Kasulu katika Pori la Kagera Nkanda katika ziara ya Mheshimiwa Rais aliwaruhusu wananchi wale wafanye shughuli za kilimo pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara baada ya Mheshimiwa Rais kuondoka, wananchi walianza shughuli ile ya kilimo, lakini baadaye wananchi wale wamekuja kuingiliwa na kukatazwa na viongozi wa Mkoa na Wilaya. Kwa hiyo, tunataka kujua kwamba nchi hii nani mwenye mamlaka ya kupinga amri ambayo imetolewa na Mheshimiwa Rais? Tunaomba wananchi wetu wa Kasulu wa Pori la Kagera Nkanda wapewe fursa ya kuendelea na kilimo kwa sababu ni haki yao ya msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda pia kuchangia kuhusu suala zima la ardhi. Ardhi yetu imegawanyika katika maeneo mengi, hata ukiangalia kwenye sheria zake, kuna wenzetu hawa wa Land Use Planning, inaeleza kabisa kwamba tutakuwa na ardhi kwa ajili ya agriculture, tutakuwa na ardhi kwa ajili ya wafugaji, tutakuwa na ardhi kwa sababu ya reserve, tutakuwa na ardhi ya forest, tutakuwa na ardhi ambayo ni ya majanga hazard, lakini kwa nini ardhi ya wakulima mara nyingi inakuwa inaingiliwa na kusababisha migogoro?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii migogoro imekuwa haiishi wala haipungui, kumekuwa kuna interference kubwa sana, sasa kama tumetenga vitengo vya ardhi ambavyo vime-categorize ardhi kutokana na sekta mbalimbali, kwa nini wakulima katika suala zima la ukulima wanaingiliwa na wanashindwa kufanya kilimo chao kwa nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ni muhimu sana lingewasaidia wakulima wetu ni kuhusu kupata Hatimiliki ambazo ni za kisasa. Tunadanganywa hapa Bungeni kila siku kwamba Hatimiliki za Kimila na Hatimiliki za Kiserikali zina hadhi sawa katika mabenki yetu. Hili suala siyo kweli! Wakulima wanaoenda na Hatimiliki za Kimila katika mabenki hawapewi mikopo, mtu anaenda na Hatimiki ya Kiserikali anaonekana ana hadhi kuliko anayeenda na Hatimiliki ya Kimila. Wakulima wetu huko vijijini wanaenda kubalidishana mazao yao na chumvi, wanabasdilishana mazao yao na bodaboda, wanabadilishana mazao yao na nguo, wanabadilishana mazao yao na yeboyebo. Kwa nini Serikali isiweke mpango kabambe wa ardhi wa kuhakikisha kwamba hata ardhi za vijijini sina pata granted right of occupancy ili na wao waweze kuwa na hadhi sawa na watu wengine ambao wanapata mikopo na wasiendelee kubadilishana mazao zao na kuku na vitu vingine vinavyoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudi kwenye zao la mchikichi Mkoa wa Kigoma. Miaka ya 1970 Mkoa wa Kigoma tuliwapa zao hili mbegu nchi ya Malaysia na Malaysia sasa hivi inafanya vizuri kwenye zao hili kuliko kitu chochote, kwa nini Serikali sasa isiunde Kituo cha Utafiti ili waweze kutafiti zao hili na kuweza kutusaidia wakazi wa Kigoma. Wenzetu Burundi ukifika mpakani pale mwa Kigoma ukianza Burundi mpaka unafika Makao Makuu ya Mji wa Burundi nchi yote imepandwa michikichi, kwa nini mnashinda kuendeleza zao la mchikichi katika Mkoa wa Kigoma? Ningependa kupata majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Wilaya yetu ya Kakonko tuna mazao ambayo tunalima, tuna mahindi, mihogo, mpunga, karanga lakini mazao ya biashara tuna tumbaku, kahawa na pamba. Serikali ina mkakati gani wa kuhakiksha kwamba mazao haya yanapatiwa ufanisi ili yaweze kusaidia katika sekta nzima ya Ardhi?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta nzima ya kilimo inahusisha sekta nzima ya maji, huwezi kufanya kilimo bila kuwa na maji. Kwa hiyo basi, kwa sababu katika Wilaya yetu na Kakonko na maeneo mengine tumekuwa tukipokea Wakimbizi na kuna makambi mbalimbali ya wakimbizi hali ambayo inapelekea wakimbizi wale wakihitaji sekta ya nishati…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)