Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Manispaa ya Iringa ina mradi wa machinjio ya kisasa ambao Kitaifa ni wa pili kwa ubora na una uwezo wa kuchinja ng‟ombe 100 na mbuzi 100 kwa siku, mradi huu umebaki kidogo kumalizika kutoka Serikali Kuu. Manispaa ya Iringa iliomba shilingi milioni 200/= ili kumalizia, gharama ya mradi ni bilioni moja. Hadi leo hii fedha hiyo haijatolewa hata senti na iliomba bajeti ya mwaka 2015/2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huo ukimalizika, ajira zitaongezeka kwa vile machinjio hiyo ina uwezo wa kuajiri watu 200. Naomba Waziri anijibu: Je, katika bajeti ya mwaka 2016/2017 mradi huo umeutengea fedha kama Manispaa ilivyokuwa imeomba?