Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Wizara ya Kilimo kwa kujitahidi kutuletea mpango mzuri ambao kazi yetu sasa ni kujaribu kuonesha namna ya kuboresha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ibara ya 239 ukurasa wa 99 Mheshimiwa Waziri ameanza vizuri, ameanza kwa kuanza kwa kutupa mihimili minne ambayo sasa ataitumia katika kuendesha kilimo. Kwa umuhimu wake ninaomba ninukuu muhimili wa nne ukurasa wa 129 anasema anakwenda; “kuweka mfumo mpya wa usimamizi wa kilimo, kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi kwa uendeshaji kibiashara na kuwezesha wakulima kuwa na sauti katika uendeshaji na biashara ya mazao yao.” Mwisho wa kunukuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina budi kumpongeza sana Waziri kwa mkakati huu na kwa wale waliokuwa wanasema Waziri hatoshi mimi naomba nitofautiane nao, anatosha kabisa. Anatosha kwa sababu ametuonesha principles zake, sasa mimi naomba nioneshe matatizo ambayo nadhani yatakukwamisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha kwanza kabisa katika nchi hii labda wengi hatutambui kwamba mazao ya kimkakati kimsingi yanaendeshwa kwa sera za kikoloni ambapo mazao yale kimsingi sio mali ya wakulima, yanachukuliwa hususani kama mali ya Serikali. Jambo hili naomba litambulike na mimi nasimama hapa kwa niaba ya walionituma, wananchi wa Muleba Kusini na niseme kwamba Kagera kwa ujumla na Kanda ya Ziwa kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya kilimo katika Jimbo langu la Muleba Kusini na kusema Ukanda wa Ziwa kwa ujumla ni taabani. Ni taabani kabisa ukweli ndio huo, hali si nzuri na tukiendelea hivi bila kumuunga mkono Mheshimiwa Waziri na kuleta mawazo ya kisasa, mawazo yanaweza kuleta mapinduzi katika kilimo tutaendelea kutaabika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoona katika Ibara ya 178 wanazungumzia kwamba hatimaye watafikiria mpango wa mkakati kama wa SAGCOT kwa ajili ya Kanda ya Ziwa, mwaka jana nilisema na ninarudia kusema kwamba umechelewa Mheshimiwa Waziri, nataka kujua hiyo LAPCOT (Lake Province Agricultural Growth Corridor) inaanza lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu nchi yetu ilivyo ni vizuri kwamba SAGCOT iendelee na ni haki ni lazima tuipe nguvu lakini wakulima wa Kusini hawawalishi wakulima wa Kaskazini, hawawalishi Mikoa ya Ziwa, ninasimama hapa watu wamenituma hapa tena wananiamini kabisa neno mgomba hakuna neno mgomba katika kitabu hiki, jamani ndizi siyo chakula? tena sisi Wahaya tunasema kama ndizi haziko mezani na chakula hamna au siyo? Zao la ndizi/ mgomba umesahaulika kabisa this is not serious, hatuwezi kuwa na mpango wa kilimo ambao umesahau kabisa zao la mgomba! Hilo ni la kwanza naomba Mheshimiwa Waziri utakaposimama mimi ninaimani na wewe uje uniambie imekwendaje Mheshimiwa Tizeba imekuwa Tizijuka umesahau kabisa? Maana yake majina haya yanashabihana kwa wale ambao hawajui lugha hizi, yaani tumekwendaje. Hiyo naomba Mheshimiwa Waziri lijibiwe tujue. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mnyauko tulikuwa tunahangaika hapa na mnyauko, this is now forgotten completely hakuna hata neno lolote la kusaidia wakulima wa migomba nchi nzima, mind you hata Mbeya SAGCOT wako, hilo ni la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili niongelee ushirika kwa haraka. Ushirika nilisema wakati tunajadili bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu na nashukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu mambo mengine ambayo ameyafanyia kazi naona vijana wa TRA wanaanza kujipanga upya nashukuru sana, lakini suala la ushirika msiuchukulie kama tukio, sasa hivi Mheshimiwa Tizeba huna uwezo wa kuingia Muleba kununua kahawa yote. Ulikwenda kule nakushukuru lakini nilisikiliza ile speech yako uliyoyasema yale hayawezi kumsadia bibi kizee kama mimi ana magunia yake mawili pale mlangoni unamuambia abebe magunia apeleke kwenye chama cha msingi ambacho hakipo, ambacho kitafunguliwa kimechelewa, wakati ana uwezo wa kununua direct farm gate price kuuza kahawa yake kwa mteja wakapeleka . (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani muangalie implications za vitu tunavyovipanga vingine havitekelezeki kwa mtu anayejua hali halisi ya kijijini, naomba Mheshimiwa Waziri unahitaji time, tukupe time ya mwaka huu uandae ushirika uje next year kutuambia direct purchase, farm gate price tunafunga na inayoeleweka kusudi tuweze kushiriki. Hii hii umeshtukiza mno it can’t work! Lazima niwe mkweli kwako kwamba hapa tunapozungumza wenzangu wa Kigoma watasema, lakini kahawa imevuka. Kwa hiyo mambo haya Waziri anaenda vizuri tumuwezeshe na mwisho kabisa tumpe wataalam wa ugani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Kilimo hana watalaam, huyu Waziri he is a general without an army! Maafisa Ugani wako chini ya Halmashauri, namshukuru sana Mheshimiwa Rais hatimaye Maafisa Ardhi wamerudishwa, Mabwana Shamba ni Wataalam wamesomea hizi fani, warudishwe kwenye Wizara mama waweze kuwajibika, sasa hivi wanafanya wanalotaka huko. Kwa hiyo, Maafisa Ugani hawapo nadhani tutakwama kwa mambo haya. Kwa hayo mambo matatu na utafiti ni muhimu sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mbegu hasa nimeona hapa Agricultural Seed Agency na wenyewe wanazo tani 700 wakati nyingine zote zinatoka nje, ninaomba uwezeshe agricultural seed agency kununua sasa mbegu kwa ajili ya distribution kwa wakulima, huo ni ushauri wangu, nafikiria kwamba Mheshimiwa Waziri anafanya kazi vizuri, lakini mfumo alionao hauwezi kumruhusu kwenda mbele. Kwa sababu kama wakulima wanamiliki mazao yao basi tuwape nafasi hawa watu wakulima ambao wako kwenye fair trade watu wa kahawa ambao wako kwenye fair trade, organic trade wale waruhusu hawana haja ya kuja kwenye mnada wa Moshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnada wa Moshi kile ni kituo cha mazao tu mnada huko London na New York, kama unataka kupata bei nzuri auction zipo London zipo New York pale Moshi tunafanya coordination tu na coordination inaweza ikafanyika pia kwa kutumia farm records. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nafikiria kwamba wataalam wako Mheshimiwa Waziri wakupe proper analysis ya mambo yalivyo wengine humu tunayaelewa, tuko tayari hata kusaidia, lakini ukija na vitu ambavyo havitekelezeki, kwa mfano ukisema kwamba kwa dharura unazuia watu kuwasaidia wakulima itakuwa shida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache atakaporudi naamini kwamba tutaelewana.