Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na mimi kwa kupata nafasi hii niweze kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli kilichotokea kwenye nchi hii na kinachoendelea yako mambo ya ajabu sana, wakati Serikali hii ya Awamu ya Tano imeingia madarakani ilisema kwamba ni Serikali ya wanyonge, lakini huwezi kuamini kinachotokea, bajeti zinatengwa kila mwaka lakini utekelezaji wake haujawahi kuzidi asilimia 20. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka uliopita 2016/2017 ilitengwa bilioni mia moja na moja lakini fedha iliyokwenda kufanya shughuli za maendeleo ilipelekwa bilioni tatu. Mwaka 2017/2018 imetengwa bilioni 150 lakini fedha iliyokwenda kutekeleza majukumu ya maendeleo kwenye kilimo ni shilingi bilioni ishirini na saba ambayo ni sawa na asilimia 18.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema kwamba hii ni Serikali ya wanyonge huu ni uhuni kwa Watanzania, Watanzania wanasikitika kupita kiasi, wanaona kama wamepata mkosi kwa sababu ya Serikali hii. Haiwezekani kabisa hii Serikali siyo Serikali ya wanyonge imekuwa ni Serikali ya watu asilimia tano wenye kipato cha chini na kipatao cha juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii asilimia tano ya Watanzania ambao wanauwezo wa kupanda ndege ndiyo ambao wamepewa kipaumbele katika nchi hii, leo hawa watu ambao wa wana uwezo wa kupanda ndege katika Taifa hili wanaendelea kununuliwa ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zimenunuliwa ndege tano kwa mkupuo na juzi wanasema wameongeza ndege ya sita kwa ajili ya kuhakikisha kwamba watu asilimia tano ambao wako katika Taifa hili wenye uwezo wa kununua magari, wenye uwezo wa kufanya kazi, wenye uwezo wa kujenga nyumba nzuri, lakini wale watu maskini wote wamesahauliwa kabisa. Jambo hili linasikitisha sana. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimjibu kwamba taarifa yake siipokei kwa sababu hata fedha za afya ambazo zinakuja kwenye bajeti yetu ni fedha ambazo zinatoka nje. Fedha za ndani hakuna fedha yoyote inayokwenda kwenye Wizara ya Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba Mawaziri wakae watulie, kazi yetu sisi kama Wabunge ni kuishauri Serikali. Sisi hapa hatugombani na Serikali bali tunaishauri iweze kufanya kazi vizuri lakini watu wanaomba taarifa ambazo hazitaweza kuisaidia nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba Serikali hii haijajipanga kuhakikisha kwamba maisha ya Watanzania yanakuwa bora. Watanzania asilimia 80 ambao ni maskini ambao ni wakulima na wafugaji wamesahaulika kabisa katika Serikali hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado naendelea kusisitiza Serikali hii ni Serikali ambayo imekuwa tofauti kabisa na Serikali zilizopita, ni Serikali ambayo haiwajali wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka kipindi cha Mheshimiwa Mkapa wakulima waliweza kuenziwa sana, walipelekewa pembejeo na walilima. Kipindi cha Mheshimiwa Jakaya Kikwete tumeona hali halisi ilivyokuwa kwenye bajeti ambazo zinaonekana kwenye taarifa za fedha mbalimbali kwa miaka ya nyuma lakini Serikali hii imekuwa Serikali ya vitu na siyo Serikali ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa tunakoelekea watakwenda kuwauliza mwaka 2020 na kama mnafikiri wananchi wa miaka ya nyuma ndiyo wananchi wa sasa hivi, hawa wananchi wanaona na wanasikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna mawakala wetu walioweza kusambaza mbolea miaka iliyopita leo mnasema mnafanya uhakiki wa mawakala wetu kwamba wamedanganya, hivi mawakala wote nchi nzima ni wezi? Kwa nini tunaendelea kuishauri Serikali kwamba iendelee kuwaamini Watanzania, iendelee kuwaamini wananchi wake hamtaki kuelewa jambo hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda bado kwa sababu nimeibiwa muda. Nataka kusema mawakala wetu wapatiwe fedha zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tumepata taarifa kwamba wanataka kutuletea mbolea ya Minjingu. Mbolea ya Minjingu kwenye Nyanda za Juu Kusini ni mbolea ambayo haikubaliki kabisa, imeshindikana. Tuliwahi kutumia mbolea hii lakini tulipata hasara kubwa. Tunaomba mbolea hiiā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)