Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Naibu Waziri wake Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa na timu ya Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe unafahamu kama tuna Wizara ambayo ina idadi kubwa ya wasomi ni Wizara ya Kilimo. Waheshimiwa Wabunge huo ndiyo ukweli, hizi changamoto naziona na mmezisema vizuri sana, upande wa bajeti mmeisema vizuri sana, sasa sisi ni Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nadhani badala ya kwenda kwa anachopendekeza Mheshimiwa Bashe, tuangalie kanuni zetu. Kanuni ya 105 inatoa fursa zile siku za mwisho baada ya mjadala wa Wizara zote Serikali na Kamati ya Bajeti wafanye majadiliano eneo hili la kilimo liwe miongoni mwa maeneo ambayo tunadhani yaangaliwe. Nadhani tukienda hivyo, tutakuwa tunaenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, mmesema vizuri maana tunaiona development budget ya Wizara hii inaenda chini lakini hotuba ya Waziri ina maeneo mengi mazuri sana, sina muda wa kuyasema lakini eneo la umwagiliaji, nchi hii kwenye mabonde lakini tukienda kwa sera yetu na mikakati yetu angalau tuelekee katika kupata hekta milioni moja ambazo tumejiwekea, sasa hii imekuwa ni ngonjera tu. There is a big disconect kati ya Wizara ya Fedha, Wizara ya Umwagiliaji na Wizara ya Kilimo katika mikakati yetu lakini tukienda kwa pamoja tutafanya vizuri. Kuna maeneo mengi ya nchi hii ambayo ni kukinga maji tu ya mvua haya Mwenyezi Mungu anatupa, kuyakinga na kuyatumia kwa shughuli za umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda niongelee kuhusu pamba. Mimi nimekulia kwenye zao hili la pamba na Victoria Federation ilikuwa inafahamika, Afrika nzima walikuwa wanakuja kujifunza Tanzania. Sitaki kurudi kwenye historia, tulivuruga sisi wenyewe lakini nasema hivi mimi kama kiongozi wa Bariadi sitakubali utaratibu unaopendekezwa na Serikali wa kulazimisha ushirika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamba kwetu ni siasa kali, pamba ni uchumi, pamba ni hali yetu ya maisha. Ushirika ni kitu kizuri sana ndiyo nimeanza nalo, tulikuwanao, tulipambana na Wahindi na Waganda ndiyo tukaanzisha shughuli zetu, lakini haikuwa suala tu la kulima na kuuza pamba, uchambuzi wa pamba, zile ginneries zote zilikuwa za wakulima. Sasa huwezi ukanidanganya mimi pamba nikuletee eti kutoka kwenye AMCOS halafu iende kwa mtu private, ulishasikia ni ushirika huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja lakini siyo kwa hoja hiyo.