Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa ya kuchangia Wizara hii ya Kilimo. Wizara hii ni muhimu sana hususani kwa sisi Wabunge ambao tunatoka kwa waathirika wakubwa wa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siko mbali na wale waliozungumzia bei ya pamba. Kama umesikiliza Wabunge wengi wanazungumzia bei ya pamba, mwaka jana tuliuzia shilingi 1,200 na mwaka huu ni shilingi 1,100. Ikumbukwe kwamba wakati tunauza pamba shilingi 1,200 bei ya nondo ilikuwa ni shilingi 9,000 leo tunauza pamba shilingi 1,100 bei ya nondo ni shilingi 22,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kuonesha namna ambavyo mkulima huyu anaendelea kudidimizwa kana kwamba analima kwa ajili ya chakula cha dagaa. Sisi tulitamani kwamba wakulima wanaolima zao la pamba lengo lao ni kubadilisha maisha ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba nzuri. Cha kushangaza Serikali ndiyo imekuwa muumini mkubwa wa kuhakikisha kwamba wakulima hawasongi mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niungane pia na Wabunge waliosema kwamba suala la ushirika halina tija yoyote kwa wakulima. Serikali imetangaza kufufua ushirika lakini haina mtaji wowote wa kuendesha ushirika. Wakati Waziri Mkuu amekwenda Mwanza alikutana na wafanyabiashara, masikitiko yangu ni kwamba nilitarajia badala ya kukutana na wafanyabiashara angekutana na wakulima wenyewe ambao ndiyo wahanga wakubwa wa tatizo hili la kilimo cha pamba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetangaza ushirika, mnaagiza kwamba yale mashirika yanayonunua pamba eti ndiyo yapeleke fedha kwenye huo ushirika halafu ndiyo yanunulie pamba za makampuni yale yanayonunua pamba, hili ni jambo ambalo halikubaliki. Wakati tunazungumzia historia ya kuua ushirika maana yake ni kwamba walioua ushirika hawajachukuliwa hatua yoyote ile, lakini leo mnataka tena kuchukua fedha za wafanyabiashara wa haya makampuni wanaonunua pamba maana yake ni kwamba muwaangamize hawa wafanyabiashara kwa lengo la kuua mitaji yao, hii haikubaliki hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Bunge lililopita tulipitisha hapa kwamba msimu wa pamba uanze tarehe 1 na ndivyo ilivyokuwa, lakini mpaka hivi ninavyozungumza hakuna pamba yoyote iliyoanza kununuliwa. Hainunuliwi kwa sababu ya hili suala la ushirika la kutaka kupeleka fedha kwenye ushirika ili waweze kununua hizo pamba sasa wafanyabiashara wamegoma kupeleka fedha zao. Nachotaka kusema sasa, Serikali kama inataka suala la ushirika liendelee pelekeni fedha zenu ili muendelee kununua kwa njia ya ushirika na siyo fedha za makampuni yaliyoko kule Mkoani Simiyu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe masikitiko yangu, kuna watu wamechangia hapa kuhusu zao la mihogo na kuna taarifa kwamba Serikali hii imeingia mkataba na Wachina kwa ajili ya kupeleka mihogo lakini utashangaa hakuna sehemu kwenye hiki kitabu cha Waziri pameandikwa kitu kinaitwa muhogo. Ukitoka hapo nje kuna watu wamekuja kwa ajili ya kutetea kilimo cha muhogo. Hii ni aibu ndugu zangu kwamba watu wametoka mbali kwa ajili ya kuja kutetea zao lao la mihogo, halafu halimo hata kwenye kitabu hiki, ni mambo ya kusikitisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe kwamba kama Serikali inataka suala la ushirika liendelee pelekeni fedha zenu kuliko kutumia fedha za wakulima na kitendo cha kuwagombanisha makampuni ya pamba na wakulima kwamba wasionane nao na badala yake wakauze kwenye ushirika hilo halikubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.