Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri Mwigulu kwa kazi yake nzuri ya kutusaidia sana kutatua changamoto mbalimbali Jimboni kwangu, nina mchango ufuatao kwa Wizara:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo cha zao la pamba kimekuwa kikisuasua sana kutokana na uwepo wa changamoto nyingi kwenye zao hili. Ubora wa mbegu ya pamba unakatisha tamaa. Tunaiomba Serikali sasa iweke kipaumbele kwenye uzalishaji wa mbegu bora za pamba.
Mheshimiwa Naibu Spika, msimu uliopita Wilaya ya Bukombe ilikuwa na mnunuzi mmoja tu wa pamba, jambo lililofanya bei ya pamba kukomea sh. 800/= kwa kilo. Naiomba Serikali itoe maelekezo ili uwepo wa soko huria wauone pia Wanabukombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, wapo wakulima ambao waliingia kilimo cha mkataba, lakini kutokana na hali ya hewa, kuna mazao yaliharibiwa na hivyo kuwafanya wakulima hawa wawe na deni ambalo itakuwa vigumu kulilipa. Naiomba Serikali iweke utaratibu wa kutoa fidia kwa wananchi ambao mazao yao yameharibiwa na mvua.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa mipya, lakini Ofisi ya Kilimo Mkoa, haina gari. Naiomba Serikali itupatie gari la Idara ya Kilimo Mkoa wa Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, usambazaji na utoaji wa pembejeo uzingatie majira halisi ya kilimo. Kumekuwa na mazoea ya kuleta pembejeo nje ya muda wa msimu wa kilimo. Nashauri Wakala wa Mbegu uimarishwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, ufugaji wa samaki ni jambo linalopaswa kupewa kipaumbele sana. Serikali sasa ianze kutoa ruzuku kwa ufugaji wa samaki. Aidha, Serikali pia ianzishe utoaji wa elimu ya ufugaji samaki.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Mifugo ina changamoto nyingi. Mifugo haina maeneo ya malisho, Wilaya ya Bukombe haina maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mifugo. Naomba Wizara ishirikiane na Wizara nyingine kutenga maeneo ya wafugaji. Huduma za ki-veterinary sasa zifufuliwe ili mifugo mingi iweze kupata huduma ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.