Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iweke kipaumbele juu ya ulipaji wa mawakala na kuwaokoa na udhalilishaji unaofanywa na mabenki. Nashauri Serikali kuhakikisha haizuii uuzaji wa mazao ya kilimo bali itoe maelekezo ya kuhifadhi baadhi ya chakula ili kutoangukia kwenye njaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuongeza fedha za utafiti wa vituo vyetu, kwa mfano Vituo vya Utafiti vya Mlingano, Ukiriguru na Naliendele ili itoe matokeo yatakayoleta ufanisi katika kilimo. Pia niishauri Serikali kuhakikisha inaangalia zaidi katika suala zima la ushirika nchini kwani hakuna watumishi wa kutosha tangu walipostaafisha watumishi kwa manufaa ya umma hawakuajiri watumishi wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuangalia umwagiliaji kwenye mashamba yetu, kwenye mito yetu mfano Mwalimu Nyerere alianzisha shamba la mpunga Ruvu ambalo sasa hivi linapimwa viwanja tu na umwagiliaji uko mahututi. Niishauri Serikali kufufua mashamba haya badala ya kufanya maji haya kupotelea baharini.