Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Namtumbo na mimi mwakilishi wao tunaiunga mkono hii hoja kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kwa niaba ya wananchi wa Namtumbo kukuomba radhi kwa kauli ya kiongozi wetu wa Wilaya aliyedai eti Mheshimiwa Waziri wa Kilimo pamoja na sisi viongozi wa Wilaya ya Namtumbo wa Chama na Serikali tunawadhulumu wakulima wa tumbaku kwa kuwakopesha mbolea kwa bei ya juu tofauti na iliyotangazwa na Serikali na kwa kuwacheleweshea mbolea hiyo. Tumempuuza kwa sababu najua kabisa na wala hataki kujua utaratibu wa msimu wa kilimo cha Tumbaku ulivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri ili aelewe vizuri tatizo tulilonalo kiongozi wetu huyo wa Wilaya alitembelea mashamba ya mpunga yanayolimwa na wakazi wa Kata ya Mchomono na alipoona mpunga ulivyostawi akadhani ni magugu na akatoa amri magugu hayo yateketezwe kwa kutumia kemikali ya kuunguza magugu iliyotolewa na NGO ya PAMS Foundation ya Wajerumani na Wajerumani hao walitoa dawa husika na ikanyunyiziwa kwenye mashamba ya wakulima hao wa mpunga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hao hawajui wataishije kufuatia tendo hilo la kiongozi wetu Luckiness Adrian Amlina, DC wa Namtumbo. Nikuombe utumie nafasi yako kumjulisha Mheshimiwa Rais atuondolee adha hii ili wananchi wa Namtumbo waendelee kuishi kwa kutegemea mavuno ya mashamba yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Mheshimiwa Dkt. Charles Tizeba, Waziri wa Kilimo tunashukuru kwa kutuwezesha kumpata mnunuzi wa tumbaku ya Moshi, Kampuni ya Premier Leaf Tanzania Limited. Ulitoa kibali kwa kampuni hiyo kusafirisha green leaf nje ya nchi kwa miaka miwili kwa masharti kuwa katika kipindi hicho wajiandae kuchakata tumbaku nchini na maandalizi wameanza kwa kushirikiana na SONAMCU kufufua kiwanda cha kusindika tumbaku cha Songea. Ungekosa kutoa kibali kile kampuni hiyo haingeingia mkataba wa kununua tumbaku Namtumbo na Songea na hivyo kutuwezesha kulima tumbaku mwaka huu na miaka itakayofuata na hivyo kufufua zao hilo la kibiashara na la muda mrefu huko nyuma. Mwezi ujao tu pesa zitaingia Namtumbo kupitia kufufuliwa kwa zao hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri udumu kuhudumu katika Wizara hii. Amina!