Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshiwa Mwenyekiti, naomba nichangie Wizara hii muhimu sana na ndiyo uti wa mgongo wa Taifa kwani ni zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania ni wakulima na ndiyo wanapata kipato chao. Wizara hii inategemewa sana tumaini la viwanda vya Tanzania vinavyotarajia kupata malighafi za kuendeshea viwanda vyao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pembejeo imekuwa ni tatizo kubwa sana kuna mikoa yenye misimu miwili na mikoa yenye msimu mmoja. Lakini sote tunatambua kuwa wakulima wengi wanaanza kuandaa mashamba mwisho wa mwezi wa nane au mwazo wa mwezi wa tisa. Lakini pembejeo hadi wakulima wamemaliza mashamba na mazao yameanza kuota hakuna pembejeo iliyopelekwa. Niombe Serikali chonde chonde tupelekeeni pembejeo kwa wakati ili wakulima wapate pembejeo za kupandia na kukuzia kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mbegu za ruzuku, huko nyuma tulikuwa na utaratibu wa kutoa mbegu za ruzuku mfano, mahindi, mpunga alizeti, choroko, kunde na kadhalika. Leo hii mbegu hizo za ruzuku hazipatikani, niombe sana kwa Mheshimiwa Rais anataka viwanda vya mafuta vya ndani kwa nini sasa tutoe ruzuku msimu wa 2018/2019 kwa mbegu zifuatazo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, alizeti, ufuta, michikichi, michikichi, niombe Serikali kwa kuwa Malaysia ilikuja kuchukua miche ya michikichi kutoka Kigoma. Kwa nini Serikali sasa isiombe Serikali ya Malaysia irudishe mbegu, miche ya michikichi ili basi na wakulima wa Mkoa wa Kigoma wanufaike na mbegu hizo kutoka Malaysia. Sambamba na hilo, tunaweza pia kuchukua mbegu za michikichi kutoka Burundi ili basi tuwe na aina tatu za aina ya michikichi ya kutoka Naliendele, Burundi, Malaysia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa na tatizo kubwa sana kwenye zao la tumbaku kwa wakulima wa Tarafa ya Nguruka, Kata ya Basanga, Itebila, Mganza na Nguruka, mfano kucheleweshwa, kutokana kwa makisio ya uzalishaji wa kilo na makampuni waliyoingia mkataba na wakulima, kwa mujibu wa sheria ya makisio yanatoka mwezi wa tatu na mwezi wa nne, hadi leo bado tunasikia makisio hayo ya kutoka mwezi wa Septemba, 2018. Kwa kuchelewesha makisio hayo kutasababisha mambo yafuatayo:-

Kwanza, kuchelewa kuagiza pembejeo, makisio hayo kutolewa mapema ndiyo benki wanajua wamekopesha wakulima kiasi gani, kwa kuchelewa kuna sababisha mkulima kulima chini ya kiwango cha makisio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la masoko, wakulima wamelima mazao mengi, mahindi, maharage, mbaazi mpunga na kadhalika. Tatizo kubwa ni soko, tuombe Serikali iwaruhusu wakulima kuuza mazao yao nje. Tanzania iko kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa nini sasa wakulima wasiruhusiwe kuuza mazao nje ya nchi hususani ndani ya nchi ndani ya nchi za Shirikisho la Afrika Mashariki. Kitendo cha kuwazuia wananchi kuuza mazao yao nje ni kosa kubwa wakulima hawa wanasomesha watoto wao, watoto hawapewi pesa wakati na Serikali mmekataza mazao yasiuzwe nje ya nchi hii ni tatizo kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niombe kumshauri Mheshimiwa Waziri sisi Wabunge wa Majimbo ndiyo wawakilishi wao, anapofanya ziara kwenye majimbo yetu tunapomtafuta tunahitaji kumpa changamoto zaidi za wakulima wetu, sasa anaacha kutupa taarifa za ziara zake ndani ya majimbo na kuacha kuwasiliana na sisi, matokeo yake anasema ya kwake na kupokea changamoto chache, changamoto kubwa za wananchi walio wengi hazipokei, tunaomba sana, atambue umuhimu wa Wabunge wenzake wa Majimbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.