Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Njombe Mjini sasa wamepata zao la parachichi ambalo wananchi wamelipokea vizuri sana kila mwananchi sasa anashughulika na kilimo hiki. Wananchi hawa wa Jimbo la Njombe Mjini wanahitaji msaada kidogo sana wa Serikali, katika upatikanaji na usambazaji wa miche bora. Zao hili limepata soko kubwa sana nje ya nchi na hii itasaidia sana nchi yetu kuongeza pato la fedha za kigeni. Katika mauzo ya zao la parachichi nyenzo muhimu sana ni pack house (cold storage) ambazo mkulima hana uwezo wa kujenga na wanunuzi hawawezi kujenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iangalie hili na inipe maelezo kwa niaba ya wakulima wa parachichi wa Jimbo la Njombe Mjini ni kwa namna gani inaweza kusaidia hili, Wizara iunde timu ya wataalam kusimamia kuendeleza zao la parachichi na kupima vihatarishi vyake ili tuweze kusaidia zaidi utaratibu wa masoko na mauzo kwa manufaa ya wakulima na nchi kupata fedha za kigeni.