Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono mikakati mbalimbali inayochukuliwa na Wizara hii. Natambua changamoto nyingi zilizo mbele katika kutekeleza mikakati hii. Naunga mkono hoja kwa kusisitiza yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo ndiyo uti wa mgongo na unahitaji kupewa kipaumbele kwa kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo zote zinazohitajika kwa wakati; lakini vile vile tunapozungumzia viwanda hapa nchini ni lazima tujue kwamba viwanda vinategemea mazao yatokayo shambani (kilimo).
Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu kwa maana ya barabara ni muhimu sana kwani mazao hayo kutoka mashambani, ili yafike kiwandani kwa gharama nafuu, ni lazima yapite kwenye barabara zinazopitika kirahisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia viwanda ni muhimu ili mazao yetu yapate soko la uhakika. Ndani ya Jimbo la Chilonwa tunalima sana zao la zabibu, lakini soko lake ni baya sana kwa kuwa, hakuna kiwanda cha uhakika cha kuweza ku-process zabibu. Naomba Wizara hii isaidie kuweka msukumo kwa Wizara za TAMISEMI na Viwanda kuweza kuharakisha ujenzi wa kiwanda cha uhakika cha ku-process zabibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha, naunga mkono hoja.