Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote sina budi kumshukuru Mwenye - Enzi – Mungu, mwingi wa rehema kwa kuniwezesha kuchangia hapa hoja iliyopo mezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ninapenda nikupongeze wewe mwenyewe kwa namna unavyosimamia Bunge hili kwa umakini mkubwa sana. Ninaomba nizungumzie mambo yafutayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mazao ya mahindi na mbaazi, msimu huu mazao haya yamepatikana kwa kiasi kikubwa, ni hawa wakulima wetu wamelima kwa ajili ya mahitaji tofauti kama kujikimu, kusomesha, kutibu watoto, kujenga na kadhalika, hivyo inakuwaje wananchi wanazuiliwa kuuza mazao yao nje ya nchi? Si jukumu lao wananchi kuhakikisha kwamba nchi ina chakula cha kutosha, huu ni wajibu wa Serikali. Hivi sasa mbaazi zinauzwa shilingi 100 hadi 150 kwa kilo moja, wapi tunakwenda? Mahindi nayo hayana soko, hayatakiwi. Ni vyema Serikali ikafikiri zaidi kuhusu suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuje kwenye zao la kahawa, ni vyema tungeongeza nguvu kwenye zao hili, tulikuwa tukipata fedha za kigeni. Ni vyema Serikali ingesimamia kwa umakini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ya kuweka pembejeo na mawakala, mawakala wa pembejeo wametiwa umaskini na Serikali bado imekaa kimya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu korosho, mpaka sasa hatujawa na soko la uhakika la korosho. Ni vyema Serikali ingehangaika ili kuhakikisha kwamba tunapata masoko ya uhakika kwa wakulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kusimamia wakulima, ni vyema Serikali ikasimamia kwa umakini mkubwa kuhusu wakulima, si waachiwe walime tu. Ni vyema wakasimamiwa ili waweze kulima na tija iwe kubwa zaidi, matumizi ya ardhi kuhusiana na kilimo bado yako chini sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vyema Serikali ikahangaika kutafuta masoko ya kuuzia bidhaa zetu ndani na nje ya nchi yetu. Wakulima wamekuwa wanavuna mazao yao kwa wingi ila hawana pa kuyauza, yanawaozea mikononi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, si vyema Serikali kubaki na maneno tu. Watu wanaumia, hawana pa kuuza mazao yao. Ni hatari, yanawaozea mikononi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.