Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya kilimo mwaka 2018/2019 Serikali ya CCM haina dhamira ya dhati kuendeleza kilimo na haina mpango wa kuwasaidia wakulima. Lengo la MKUKUTA lilikuwa kwamba sekta ya kilimo ikue kwa asilimia sita mpaka asilimia nane kwa mwaka kwa miaka 10 mfululizo ili Watanzania wa vijijini waondokane na umaskini. Hata hivyo hali halisi ni kuwa kati ya mwaka 2011 – 2015 sekta ya kilimo ilikuwa ni wastani wa asilimia 3.4 kwa mwaka. Mwaka 2016 na 2017 miaka miwili ya Serikali ya Awamu ya Tano kilimo kilikua kwa asilimia 19 mwaka 2016 na 2017 ni asilimia 1.3.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uzalishaji wa mazao yote makuu isipokuwa korosho umeshuka katika mwaka 2016/2017; kahawa uzalishaji umeshuka kutoka tani 760,000 mwaka 2015 mpaka tani 48,000 mwaka 2017; pamba imeshuka kutoka tani 50,000 mwaka 2015 mpaka tani 48,000 mwaka 2017; tumbaku imeshuka kutoka tani 87,000 mwaka 2015 mpaka tani 61,000 mwaka 2017 na chai imeshuka kutoka tani 33,000 mpaka tani 27,000 mwaka 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata mazao ya chakula; wakati mahindi uzalishaji umeongezeka kutoka tani milioni 6.1 mwaka 2016 mpaka tani milioni 6.6 mwaka 2017, bei ya mahindi imeporomoka sana kufuatia Serikali kuzuia mahindi kuuzwa nje ya nchi na Serikali yenyewe kutonunua mahindi kwa ajili ya ghala la Taifa. Hii ni kwa sababu NFRA haikuwepewa fedha za kununua mahindi na hivyo Serikali kuwapa umaskini wananchi na wafanyabiashara wa mazao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya Wizara ya Kilimo imezidi kushuka, kwa mfano mwaka 2017/2018 pesa zilizoidhinishwa na Bunge zilikuwa shilingi bilioni 221.10. Mwaka 2018/2019 Wizara inaomba kuidhinishiwa na Bunge shilingi bilioni 170.27, hii ni pungufu ya asilimia 23 kulingana na bajeti ya mwaka jana. Hii sio sawa ukizingatia umuhimu wa sekta hii ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kushauri mambo yafuatayo:-

Moja, kwa ajili ya kujenga uchumi shirikishi ni muhimu kufanya jitihada za makusudi kuhakikisha kwamba kilimo chetu kinaanza kuchangia vya kutosha katika ukuaji wa uchumi. Serikali iweke shabaha ya kufuatilia ukuaji wa asilimia nane wa sekta ya kilimo.

Mbili, Serikali lazima itambue kuwa kilimo ndiyo shughuli kuu ya kutokomeza umaskini. Shughuli za kilimo ziendeshwe na wananchi wenyewe kwa kuwawezesha kumiliki ardhi, kuongeza tija na kupata mitaji.

Tatu, Serikali itunge stable fiscal regime katika sekta ya kilimo na kuhakikisha kwamba mkulima anabaki na sehemu kubwa ya mapato baada ya mavuno ya mazao yake.

Nne Serikali iunde mamlaka ya kilimo itakayosimamia sekta ya kilimo na kutekeleza mikakati yote ya maendeleo ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano na mwisho, Serikali ihusike kikamilifu kwenye uhifadhi wa mazao kupitia soko la bidhaa (commodities exchange) ambao utashirikisha vyama vya wakulima na hivyo kufuta middle men.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.