Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mara nyingi mvua za kwanza ni za kupandia. Hivyo basi naomba Serikali iwe inawafikishia wakulima mbolea ya kupandia mapema kabla ya mvua za mwanzo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo mawakala waliofanya kazi ya kusambazia wakulima mbolea na mpaka sasa hawajalipwa pesa yao. Kwa vile Serikali ilishafanya uhakiki, kwa vyovyote ilishabaini ukweli uko wapi. Hivyo, naomba wale waliofanya kazi kwa uaminifu waweze kulipwa na wale waliodanganya wasilipwe, wengi wanapoteza maisha yao kwa sababu ya kudaiwa na mabenki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno haya, naomba kuunga mkono hoja.