Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ni muhimu kwa maisha ya watu na kiuchumi pia, na ndiyo Wizara inayoweza kutupeleka kwenye nchi ya viwanda kwa upatikanaji wa malighafi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipeleke fedha za kutosha ili kuiwezesha Wizara hii kufikia uchumi wa kati. Ili Watanzania waweze kuishi na wawe na afya bora lazima wale chakula kinachozalishwa nchini na wakulima waishio vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na wakulima hao kulima kwa bidii bila hata msaada wa kitaalam, inafika mahali Serikali inamuwekea masharti mkulima huyo namna ya kuuza mazao yake. Huu utaratibu haukubaliki na unakandamiza mkulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ardhi tuliyonayo ni kubwa na inafaa kwa kilimo, lakini ni kwa nini Serikali haiandai mipango bora ya kutumia ardhi hiyo kuzalisha mazao ambayo yatasababisha nchi kuuza nje ya nchi. Matokeo yake Serikali inafunga mipaka kwa mazao kama mpunga, mahindi, kahawa na kadhalika na kumzidishia umaskini mkulima mdogo kwa kushindwa kuuza mazao yake na kusababisha mazao hayo kuharibikia kwenye maghala ya kienyeji. Serikali iwe na huruma kwa wananchi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mlimba ni eneo la kilimo, wananchi wanalima mazao ya biashara na chakula ambayo ni mpunga, mahindi, ufuta, ndizi, kokoa, alizeti, miti na pia ni eneo la SAGCOT lakini barabara za vijijini na barabara kuu hazipitiki kwa mwaka mzima na kusababisha mazao hayo kununuliwa kwa bei ya chini na kumuongezea umaskini mkulima. Nashauri Wizara ione haja ya kuwezesha jimbo hilo kupata pesa za kujenga masoko ya kisasa ili kupata urahisi wa kuuza mazao hayo kwa bei zinazokubalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushirika umeleta taharuki kwa wananchi wa Tanzania hususan Wilaya ya Kilombero. Viongozi wengi takribani asilimia 95 ya viongozi wa vyama hivyo wamefanya ubadhirifu wa fedha na mali za ushirika. Matokeo yake sasa eti wameunda timu ya kukusanya madeni matokeo yake, wanatoza tozo watu na viongozi walioua ushiriki ndiyo wanaoshirikiana nao. Ushahidi upo na viongozi hao walioua ushirika wapo, lakini hawajachukuliwa hatua yoyote. Hili halikubaliki kabisa.