Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna uhitaji mkubwa wa sukari na mafuta hapa nchini. Kinachohitajika ni kutengeneza mazingira bora ya kuzalisha miwa na oil seed (alizeti, ufuta na kadhalika). Naamini Serikali ikifanya kazi kwa pamoja kati ya Wizara za Kilimo, Wizara ya Viwanda na Wizara ya Fedha, kwa mfano, Brazil imefanikiwa kutokana na kuwekeza katika viwanda vidogo na vya kati, hii ni kwa sababu kuwekeza katika viwanda vikubwa inahitaji fedha nyingi lakini pia huchukua muda mrefu mpaka hata miaka mitano na ndiyo maana Wizara inayo kila sababu kutengeneza mazingira ya kuibua maeneo yanayofaa kwa kilimo cha miwa na uwekezaji wa viwanda vya sukari. Tujifunze kutoka Brazil, potential ipo kubwa na ya wazi. The same can be applied kwenye suala la mafuta ya kula. Ninaamini hata kwa kushirikiana na Wizara ya Ulinzi (JKT) tunaweza kuibua maeneo yanayofaa kulima oil seeds (alizeti) na kadhalika ili kuwa na malighafi ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini Wizara ya Kilimo iki-take lead, Taifa hili litapiga hatua na dhana hii ya uchumi wa viwanda itakuwa ya vitendo na yenye kuleta tija. Pamoja na mchango huu, naambatanisha nakala yenye kuonesha maeneo potential kwa uwekezaji wa kilimo cha miwa na uzalishaji sukari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wachangiaji wengi wamesema sana kuhusu mbolea. Ushauri wangu ni kwamba hiyo inayoitwa ruzuku, afadhali fedha yake ingetumika kufanya distribution, kwa maana kuwa isaidie ku-cover gharama za usafirishaji. Hii ni kwa sababu wakulima wanachohitaji ni mbolea kuwafikia kwa wakati. Suala la bei kwao siyo issue sana, issue ni mbolea iwafikie kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo mengi nchini ambayo tunaweza kujenga viwanda vidogo na vya kati (tani 10,000 mpaka tani 30,000 kwa mwaka). Kila mkoa una maeneo kama haya, kwa mfano, Kilosa tani 10,000; Manyara tani 10,000; Mara tani 30,000; Ruvuma tani 10,000; Dodoma – Chamwino tani 10,000; Kigoma – Bonde la Malagarasi tani 30,000; Pwani – Rufiji tani 30,000 na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uendelezaji wa viwanda vidogo unachukua muda mfupi, kama miezi minane hadi kumi. Gharama zake ni za chini USD milioni tatu hadi USD milioni 10 ukilinganisha na vile vikubwa USD milioni 100 hadi USD milioni 300 ambavyo huchukua miaka miwili mpaka mitano. Viwanda vidogo viko karibu na wananchi. Bei ya sukari yake ni nafuu kutokana na gharama kuwa chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri za Wilaya husika zinaweza kuingia ubia na wawekezaji wazalendo katika maeneo yao na miradi hii inaweza kuingizia mapato Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.