Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasita kuunga mkono hoja Wizara hii ya Kilimo kwa sababu zifuatazo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, sijaona juhudi za kuimarisha kilimo hata kidogo hasa wakulima ambao ndio wapiga kura wa nchi hii, hawajasaidiwa vya kutosha. Mbolea haipatikani kwa wakati, bei yake haieleweki, wala masoko ya mazao hayapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mbolea nashauri Serikali itumie waagizaji wa pamoja (bulk procurement system) lakini waagizaji watakiwe kwenye masharti wafikishe mbolea kwenye mikoa ya uzalishaji na kwa kiwango cha mahitaji, usambazaji uanzie pale Makao Makuu ya Mikoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri mbolea ya Minjingu isilazimishwe kwa wakulima, ifanyiwe utafiti na Serikali iiwekee ruzuku ndogo ili wananchi waitumie miaka miwili au mitatu, wakiipenda wataendelea kuitumia. Mbolea nyingine kama DAP iendelee kuwepo kwenye soko.

Aidha, mawakala walioisadia Serikali kutoa pembejeo wasidhulumiwe, wapewe kile kitakachoonekana ni haki yao. Siyo sahihi kuona kuwa mawakala wote ni wezi na hawapaswi kulipwa. Mbolea ije kwa wakati, Mkoa wa Rukwa leta mbolea mwezi Agosti mpaka Septemba. Mbegu ziwe za viwango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu masoko, wakulima wa Nkasi Kusini wanalima kwa gharama zisizolingana na soko la mahindi kwa sasa. Inakatisha tamaa. Mfumo wa commodity exchange system inaonekana unafanya vizuri. Nashauri NFRA inunue mahindi hata kwa kutengeneza siasa na hawa wakulima, ni muhimu sana. Hawa ndio waliotuamini na kutuweka madarakani. Sasa mambo yao hakuna hata moja lenye nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muujiza gani utafanyika kuinua uchumi wa viwanda huku umeacha kilimo nyuma? Hii siyo sawa kabisa, Serikali ishughulikie mambo ya wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi ambao ni wakulima wa vijiji vya Kasu, Kisura, Milundikwa na Malongwe wamenyang’anywa mashamba waliyopewa kwa utaratibu wa kawaida na sasa hawana mahali pa kulima. Zaidi ya watu 4000 wameathirika kwa jambo hili, hawaendi kulima maana wao ni wakulima na sasa watashindwa kusomesha watoto, kujenga nyumba bora, kupata matibabu bora, kuvaa nguo nzuri na kupata chakula cha afya. Serikali iangalie hili jambo.