Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba Awamu ya Pili ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo itaendelea kutekelezwa chini ya uratibu wa mipango shirikishi ya maendeleo ya sekta ya kilimo katika Halmashauri zetu n Na kwa kweli utaratibu huu utakuwa mzuri zaidi na utafanikiwa zaidi kama watu wetu watakuwa wamejitolea kusimamia vizuri kwa mujibu wa taratibu na sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo ndipo tunapoagiza na tayari Serikali imeshawaagiza watumishi hasa Maafisa Ugani na Maafisa Kilimo, wahakikishe kwamba mipango ya maendeleo ya sekta ya kilimo katika Halmashauri zetu lazima itekelezwe kwa umakini na weledi wa hali ya juu. Na tunawaamini, watumishi ambao walikuwa wamezoea kuweka kambi katika makao makuu ya Halmashauri hawawatembelei wakulima, Serikali imeshatoa maelekezo kupitia Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba lazima wawatembelee wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hii kama tutaendelea kuona kwamba kuna uzembe kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wengi wamelalamika hapa, tutaanza kuchukua hatua kali, kwa sababu maelekezo haya ya Serikali ni halali. Lazima wakulima wapate haki yao ya kupata elimu ambayo inatoka kwa watu ambao wameajiriwa na Serikali, na hawa ni pamoja na maafisa walioko katika Halmashauri, Kata na katika Vijiji, lazima wafanye kazi zao. Utaratibu wa kusubiri posho, kwamba lazima kuwe na posho ndiyo mtu akafanye kazi yake ambayo ameajiriwa kuifanya, tumeshaupiga marufuku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kupata kilimo bora kama hakuna elimu bora ya kilimo, na ndiyo maana tunawasisitiza hawa jamaa waweze kufanya kazi yao ambayo wameajiriwa kuifanya, hii ni pamoja na Maafisa Ushirika. Maafisa Ushirika wameshaelekezwa kwamba lazima Maafisa Ushirika wahakikishe wanafanya mapitio ya vyama vya ushirika vya msingi vilivyopo katika maeneo yao kuona utendaji wa vyama vya ushirika kama ni mzuri. Ili kama utendaji wao ni mbovu waweze kuvifuta na kuvisajili upya vyama ambavyo vitawasaidia wakulima. Hayo ni maelekezo halali ya Serikali na sisi tutaendelea kuyasimamia na kuyafuatilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa Ugani wameshaelekezwa wafanye mazoezi ya kuwatambua wakulima wote na mahitaji yao ya pembejeo ili Serikali ifanye maandalizi mazuri na mapema ya pembejeo, kwa hiyo hilo nalo tutaendelea kulifuatilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nadhani nisiseme sana kwa sababu mwenye sekta mwenyewe yuko hapa, wale watu ambao wako chini ya TAMISEMI waipatepate huko waliko, wajue kwamba sisi tuko macho tutaendelea kuwafuatilia kuhakikisha kwamba uzembe wa aina yoyote hautavumiliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, naunga mkono hoja.