Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ili na mimi niweze kuchangia Wizara hii ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo kama Taifa tuna-set trend ya kuwa, sekta hii ya Mifugo na Uvuvi haijaliwi na Serikali ya CCM. Kwa nini nasema hivi; tangu Serikali hii ya Awamu ya Tano iingie madarakani hakuna hata asilimia moja ya Bajeti ya Maendeleo iliyoweza kupelekwa kwenye sekta hii. Sekta ya uvuvi pekee inatoa ajira kwa Watanzania milioni tano, hii ni sawa na asilimia 10 ya wananchi wote wa Tanzania. Pia watu milioni nne wanajishughulisha moja kwa moja na shughuli za uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 7.8 ya sekta ya mifugo na uvuvi inachangia Pato la Taifa. Asilimia 5.9 ikiwa inatoka kwenye sekta ya mifugo na asilimia 1.9 ikiwa inatoka kwenye sekta ya uvuvi. Takwimu hizi zinatoka kwenye quarterly bulletin za BOT 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia sekta hii ya mifugo na uvuvi inachangia zaidi ya sekta ya madini kwenye Pato la Taifa, ambapo sekta ya madini inachangia asilimia 4.8 tu; lakini nasikitika kwamba sekta hii imepuuzwa na imeshindwa kabisa kupewa kipaumbele na Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, take it from me, tukiamua kuwekeza kwenye sekta hii ya mifugo na uvuvi na tukaweza kufikia asilimia 10 tu kuchangia kwenye Pato la Taifa nawaambia nchi hii itakimbia. Solution hapa ni ku-double tu uzalishaji na kuangalia vipaumbele vyetu ni vipi. Je, return ya investment ya ku-invest kwenye ndege ni kubwa kuliko return ya investment ya kuwekeza kwenye sekta ambayo asilimia 50 ya kaya inategemea sekta ya mifugo na uvuvi? Kwa hiyo kupanga ni kuchagua, tuamue tunachagua wanyonge ambao ni zaidi ya asilimia 90 ya Taifa hili au tunachagua asilimia tano ya watu wachache ambao wana uwezo wa kupanda ndege? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tuna ng’ombe zaidi ya milioni 28 lakini ukiangalia Botswana na Ethiopia wanafanya vizuri kuliko sisi. Hebu tukae tujiulize shida ni nini? Maldives, Mauritius uchumi wao unaendeshwa kwa uvuvi, sisi tuna tatizo gani wakati samaki wao wanakuja kwenye maji yetu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta hii kwa mwaka mmoja tu imeweza kukusanya maduhuli ya bilioni 26.9; naomba Mheshimiwa Waziri akija atueleze ni kwa nini sekta hii imeshindwa kupata pesa za maendeleo hata asilimia 10 basi wakati imeweza kukusanya kwa mwaka mmoja tu 75 percent ya malengo ya Wizara? Kwa kweli inasikitisha sana; yaani inaonesha tuna chuki, Serikali hii ina chuki kwa wafugaji, ina chuki kwa wavuvi. Hebu tuache hiyo chuki ili tuweze kuwainua wafugaji na wavuvi wa nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa pia kuzungumzia viwanda vya ndani vinavyotokana na sekta ya mifugo na uvuvi. Ningependa nianze na kiwanda cha maziwa. Viwanda vyetu vya ndani vina uwezo wa kutengeneza lita milioni 276.6 kwa mwaka, lakini sasa hivi vina uwezo wa kutengeneza lita milioni 56.3 ambayo ni sawa na asilimia 20 tu ya operating capacity.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo viwanda vyetu vya maziwa vina-operate under capacity kwa asilimia 80. Vile vile kinachoshangaza bado wafanyabiashara wa nchi hii wa maziwa na bidhaa nyingine kama cheese, butter wanaagiza bidhaa kutoka nje. Naomba Mheshimiwa Waziri akija atuambie, ni kwa nini viwanda vyetu vya ndani vya maziwa vina-operate under capacity for eighty percent (80%) yet tunaagiza bidhaa za maziwa kutoka nje na tunapoteza kama Taifa almost bilioni mia moja ishirini kwa kuagiza kutoka nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda vya nyama vina uwezo wa kusindika nyama kwa tani 626,922 kwa mwaka, lakini maajabu sasa hivi viwanda vyetu vya nyama vya nchi hii vinatengeneza au vinasindika nyama kwa tani elfu themanini na moja, elfu ishirini na mbili sawa na asilimia 13. Tuna-operate under capacity kwa asilimia 87 na bado tunaagiza nyama kutoka nje kila mwaka. Kutokana na taarifa za Wizara 2016/2017 tumeagiza nyama kutoka nje kwa kutumia dola milioni saba na bado tunasema Tanzania ya Viwanda; hivi kweli tuna nia ya dhati ya kuwekeza kwenye viwanda vyetu vya ndani au viwanda tunavyovizungumzia ni viwanda gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, ukija kwenye viwanda vya samaki. Nchi yetu ina uwezo wa ku-process tani 700,000 kwa mwaka, lakini sasa hivi capacity ni tani 350,000 tuna- operate kwa asilimia 50 tu na asilimia 50 bado tunaagiza kutoka nje. Ningependa kupata majibu yanayoridhisha kutokana na production capacity ya viwanda vyetu vya ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepitia hii hotuba ya Wizara, hotuba haiko solution oriented, haitoi solution kwa matatizo yetu. Ukisoma maneno mengi tunafanya tathmini, tumewatuma wataalam, tutajitahidi, tuta-make sure, tutafanya nini. Ukiangalia ukurasa wa 38, 39 na 40 kuonesha jinsi yeye na wataalam wake Mheshimiwa Waziri ambavyo hamko makini unasema kuhusu NARCO na NICO kwamba, naomba nianze kusoma ukurasa wa thelathini na tisa (39):-

“NARCO haikupata gawio lolote kwa kipindi cha miaka 10 na kwa kuwa hakuna maendeleo yoyote yanayofanyika kwa mujibu wa mkataba wa mipango na biashara na hivyo kutofikia malengo na matarajio ya Serikali, hivyo ili kukamilisha taarifa ya uchambuzi wa mkataba na kuiwezesha Serikali kufanya maamuzi Msajili wa Hazina anaelekezwa kufanya ukaguzi maalum (Special Financial Audit) katika kampuni ya nyama iliyopo Dodoma”.

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nikusaidie Mheshimiwa Waziri, Msajili kazi yake siyo kufanya audit. Audit inafanywa na Control and Auditor General ndiye mwenye mandate ya kufanya ukaguzi kwenye Taifa hili, Msajili kazi yake ni kuangalia mali, kwa hiyo aende aka- review hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa pia kuzungumzia suala la tozo mbalimbali na manyanyaso yanayofanywa kwa wafugaji.