Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii na nikushukuru kwa fursa uliyonipa. Kwanza kabisa, naunga mkono hoja hii asilimia miamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nianze na suala la upigaji chapa kwa sababu muda wenyewe ni mfupi. Kule kwangu Namtumbo nimepata malalamiko mengi sana ya waliopigiwa chapa. Chapa imepigwa na kuna data/taarifa fulani katika kile chuma wanachopigia chapa, lakini kila chapa iliyopigwa ng’ombe wale wameendelea kutibiwa na hakuna takwimu yoyote inayoonekana katika ile chapa zaidi ya kidonda. Kwa hiyo, hata utambuzi kwamba huyu ng’ombe ni wa Wilaya fulani haupo kutokana na namna chapa ya moto ilivyokuwa inapigwa zaidi ni kidonda tu.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi wameongelea kwamba njia inayotumika katika kupiga chapa siyo sahihi. Naomba kabisa jambo hilo lirekebishwe, itafutwe njia nyingine ya kuwatambulisha ng’ombe lakini siyo kuwachoma moto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, kwetu sisi Namtumbo eneo letu ni dogo sana, zaidi ya asilimia 67 ni hifadhi, tumeletewa ng’ombe kupita kipimo. Ng’ombe wamekuja wengi sana na matokeo yake wameleta ugomvi mkubwa sana kwa wale wakulima ambao sehemu kubwa ya Wana Namtumbo ni wakulima zaidi ya asilimia 90, inaleta ugomvi mkubwa sana. (Makofi)

Mimi sielewi, sijui kwa nini wafugaji hawatofautishi kati ya mpunga na magugu. Wanasema haya ni magugu, hizi ni nyasi, wakati ule ni mpunga. Wanasema hizi ni nyasi wakati yale ni mahindi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe sana Namtumbo hatuna eneo, wale ng’ombe ambao wameingizwa naambiwa kwamba walijazwa kwenye hifadhi, kwa hiyo walikuwa wanakula kwenye hifadhi hakukuwa na ugomvi. Kwa maana nyingine ng’ombe wengi walikuwa wanakula ndani ya hifadhi na wakulima walikuwa wanalima eneo lao. Sasa wale ng’ombe wameondolewa kwenye hifadhi wanakwenda wanavamia eneo la wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe sana tena sana mtusaidie kutatua tatizo hili. Njia pekee ya kutatua tatizo hili ni kuwaondoa wale ng’ombe au turuhusu wale ng’ombe waendelee kukaa ndani ya hifadhi kwa sababu sisi wakulima hatuingii kwenye hifadhi.