Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, tumekuwa tunashindwa kupata soko zuri la ngozi kwa sababu ya ng’ombe kutotunzwa vizuri, kitendo cha kupiga mihuri ng’ombe ni kuzidi kuharibu soko la ngozi nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, kutokomeza na ukomeshaji wa uvuvi haramu uje na mbinu na vifaa mbadala kwa wavuvi kwani hawa watu hiki ndio kimekuwa kipato chao kwa maisha yao yote.

Mheshimiwa Spika, haiingii akilini juu ya faini wanazotozwa hawa watu wanaokamatwa kwa makosa mbalimbali ya uvuvi haramu. Lazima hizi penalty zithibitishwe na sheria ya Bunge kwa kuwa zina sura ya kukomoana, lakini pia na double standards.

Mheshimiwa Spika, Wizara ilipata wapi ujasiri wa kuchoma vifaranga vidogo kiasi kile kutoka Kenya kwa madai ya uingizwaji kiholela? Kwa nini hawakurudishwa Kenya? Huu ni unyama na ni kinyume na haki za wanyama. Wizara ya Mifugo inapaswa pia kulinda haki za wanyama, kweli Wizara yako iliitia doa Serikali hii na kutufanya Watanzania tuonekane watu wa hovyo.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa samaki hawawezi kuzuiwa kutoka eneo moja kwenda na zoezi la uvuvi haramu limewekewa mkazo eneo la Tanzania Serikali/Wizara itueleze ni kwa kiwango gani kampeni hii inafanyika Kenya na Uganda kwa kuwa tunaweza kuwabana wafugaji wetu wakati Kenya na Uganda wanaendelea kuvuna.