Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na nguvu ya kuwatumikia wananchi wangu wa Kyerwa. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wa Wizara hii muhimu kwa kazi nzuri na hatua mbalimbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa; ni nzuri ingawa baadhi ya watendaji wenye nia mbaya wamegeuza baadhi ya hatua za kupambana na uvuvi haramu kuwa biashara ya kujinufaisha na uvuvi kuichafua Serikali yetu.

Mheshimiwa Spika, niishauri Serikali kusimamia vizuri sekta ya mifugo na uvuvi ili tuweze kuongeza kipato kwa Serikali yetu. Ni jambo la kusikitisha nchi yetu ina mifugo mingi, tuna maziwa na bahari zimetuzunguka, lakini hatuoni faida inayolingana na kile tulichonacho.

Mheshimiwa Spika, wafugaji wamekuwa kama yatima, hawana mtetezi yeyote. Hata pale wanapotengewa maeneo wamekuwa wakinyang’anywa, wamekuwa ni watu wa kutangatanga. Kule Kyerwa miaka ya 1987 Serikali ilitenga eneo la Sirina, Ibada 1 na Rutifa Katabe kuwa maeneo ya wafugaji na yakatangazwa kwenye Gazeti la Serikali na kupewa GN 620. Hata hivyo maeneo haya inatafsiriwa wameingia na kujimilikisha kwa kuwahonga baadhi ya watumishi wabaya na leo hii wafugaji wananyanyasika na ng’ombe, akiingia kwenye maeneo yao waliyoyapora ng’ombe wanatozwa faini ya pesa nyingi na wengine kuwakata mapanga.

Mheshimiwa Spika, nimuombe sana katika hili Mheshimiwa Waziri aingilie kati kuwaokoa wafugaji wa Kyerwa ambao wamenyang’anywa na kuonewa miaka mingi, wanahangaika kwa kutangatanga bila kupata msaada wowote.

Mheshimiwa Spika, niko tayari kutoa ushirikiano kwa Mheshimiwa Waziri kwa sababu jambo hili limekuwa kero ya miaka mingi. Kila kiongozi anayekuja ananunuliwa lakini mimi sinunuliwi kwa gharama yoyote.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya nimtakie Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri mafanikio katika vita hii ambayo watakutana na vipingamizi vingi, tunawaombea kusonga mbele mungu akiwa upande wao.

Mheshmiwa Spika, naunga mkono hoja.