Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MAULID S. MTULIA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa kunijaalia uzima na kuweza kuchangia kwa maandishi. Nawapongeza watendaji wote kuanzia Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na wote ambao sikuwataja kwa ajili ya kulinda muda.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya wafugaji wetu na Watanzania kwa ujumla. Wizara hii ikiunganishwa na Wizara ya Kilimo zina uwezo wa kuongeza ajira na kuondoa umaskini. Zaidi ya hapo Wizara hii inaweza kuondoa umaskini na utapiamlo kwa watoto wetu.

Mheshimiwa Spika, ili kufanikisha hayo inabidi tufanye yafuatayo:-

i. Kutenga maeneo ya wafugaji bila kuingiliana na wakulima.

ii. Kutoa elimu ya kutosha kwa wafugaji wetu namna bora na ya kisasa itakayowezesha kuvuna na kupata mapato ya wanyama.

iii. Wavuvi wetu waelimishwe namna bora ya kisasa zaidi ya kuvua samaki wengi.

iv. Kuanzisha viwanda vya kusindika samaki na nyama.

v. Kujenga machinjio ya nyama kwa kiwango cha kisasa ili nyama zetu ziuzwe mahotelini, migodini na hata kwenye super market za ndani
na nje.

vi. Kupunguza mifugo yetu ili tuweze kuitumia na kuwa bora.
vii. Kufuga kisasa ili kupata mifugo mingi na yenye ubora kuliko ilivyo sasa.