Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na nianze na suala la elimu ya uvuvi. Kwa kuwa wavuvi wadogo hawana uelewa wa nyavu zinazofaa na zisizofaa, ningeshauri Serikali iendelee kutoa elimu kwa njia mbalimbali kama vile tv, local radio pamoja na vipeperushi vya lugha rahisi. Pia kutoa elimu mbalimbali ya madhara ya uvuvi huo, viongozi mbalimbali na vikundi wapewe semina kwenye eneo husika na Serikali iwasaidie wavuvi wadogo wadogo wenye vikundi mitaji yenye mikopo ya riba nafuu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu upungufu wa ajira, Serikali iajiri Maafisa Mifugo kwenye maeneo mengi kwani upungufu ni mkubwa. Wafanyakazi wa Idara hizo hasa ngazi ya chini wapewe vitendea kazi kama vile pikipiki na kadhalika na madai ya watumishi wa ngazi zote yalipwe kwa wakati, kupandishwa madaraja kwa wakati kutokana na elimu zao, kusiwe na watumishi wanao kaimu kwa muda mrefu na maafisa samaki waongezwe.

Mheshimiwa Spika, wafugaji wapewe elimu ya ufugaji bora, kupunguza mifugo, kufuga kisasa, kuchungia eneo moja na kuondoa migogoro ya ardhi. Pia viwanda vya maziwa (usindikaji) vijengwe kwenye mikoa yenye mifugo mingi.

Mheshimiwa Spika, niiombe Wizara ije Mkoani Tabora kutoa elimu kwenye kiwanda cha maziwa ili kiboreshwe, ikiwezekana kuingia ubia na wawekezaji, kutafuta masoko ya mafuta ya samli, kutafuta wawekezaji wa viwanda vya nyama kwenye maeneo ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, pia kukagua machinjio mara kwa mara, usafi, upimaji mifugo inayoingia machinjioni, idadi ya ng’ombe wanaotoka safari na kuingia minadani.

Mheshimiwa Spika, madawa ya mifugo yapelekwe kwa wafugaji ili wasisumbuliwe na mawakala, kutengwe maeneo kwa ajili ya malisho, kujengwe mabwawa kwa maeneo yenye mifugo mingi na ukarabati wa mabwawa.

Mheshimiwa Spika, Serikali ione umuhimu wa kuongeza bajeti ya mifugo ili sekta hii iweze kuwa rafiki na wavuvi, wafugaji ili iweze kuboresha miundombinu. Bajeti ikiongezwa itasaidia ufuatiliaji na kero mbalimbali. Wafanyakazi kazi wapate mafunzo ya kisasa ili waboreshe elimu zao.