Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kupata nafasi ya kuchangia kwa maandishi. Nipende kusema ya kwamba sekta ya uvuvi ni rasilimali ya kujivunia sana hapa nchini kwetu na nchi yetu isingekuwa ya umaskini na kutegemea misaada kutoka nchi za nje.

Mheshimiwa Spika, naongea haya kwa uchungu sana jinsi wavuvi wanavyonyanyasika kwenye nchi yao kwa kuchomewa nyavu zao eti hazina ubora wa kuvulia, huu ni uonevu wa hali ya juu sana, otherwise Serikali itoe nyavu mbadala zinazoruhusiwa na Serikali na si kuwakamatia wavuvi na nyavu zao na kusema hazina ubora.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali iache kutumia nguvu ya dola (vyombo vya dola) kuwanyanyasa wavuvi hasa wa Mkoa wa Mara. Ukatili unaofanywa na vyombo vya dola kwa wavuvi si sahihi kabisa.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ilete nyavu zinazotakiwa kwa wavuvi wa maeneo yote na si kuwanyang’anya nyavu zao na kuzichoma halafu mnawaacha hewani.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mifugo; ukatili wa wanyama kuwekwa chapa kwenye ngozi njia inayotumiwa na Serikali si sahihi kabisa kwani ng’ombe huugua na kupata maumivu makali sana, huu ni ukatili wa hali ya juu. Haki za wanyama ziko wapi? Ubora wa ngozi unapotea, utaiuza wapi ngozi yenye alama kubwa?

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali itafute njia mbadala badala ya kuwachoma na chuma cha moto ni vema wangewavalisha ring ambazo zinakua na alama au wawekwe alama kwenye masikio na si kwa kuwachoma alama kubwa hadi kusababishia maumivu kwa ng’ombe.

Mheshimiwa Spika, hii tabia ya kutaka kupata leseni ya biashara ya ng’ombe eti lazima ujisajili Bodi ya TMB kwa shilingi 102,000 then unakata leseni ya export shilingi 2,500,000 na kila ukisafirisha mifugo ulipe shilingi 2,500 kwa kila ng’ombe mmoja (movement permit) then unalipa shilingi 5,000 kwa kila ng’ombe market fee bado shilingi 3,000 kwa kila ng’ombe kama kodi ya Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, nipende kuishauri Serikali ipunguze kodi kwa wafugaji wa maeneo yote. Nakumbuka mwaka jana baadhi ya maeneo kodi ilipunguzwa/kufutwa isipokuwa kwa mifugo tu. Ifikie mahali tumsaidie huyu mfugaji na siyo kumkandamiza.

Mheshimiwa Spika, Serikali itoe mwongozo nini mfanyabiashara wa ng’ombe anapaswa kuwa navyo ili kukidhi sifa za kusafirisha na kuuza ng’ombe ndani ya nchi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na siungi mkono hoja ya hotuba ya uvuvi na mifugo.