Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali katika jitihada zake za kuhakikisha wafugaji na wavuvi wananufaika na kazi zao wanazofanya katika kujitafutia kipato, kudhibiti uvuvi haramu, kuhifadhi mazingira na kudhibiti rasilimali za bahari na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali iweke mazingira wezeshi kwa wawekezaji katika sekta ya maziwa kwa kuangalia tozo na kodi mbalimbali zilizopo katika sekta hiyo ya maziwa. Serikali iwekeze fedha za kutosha katika uzalishaji wa viumbe kwenye maji ili kuongeza mazao hayo, kuongeza ajira na kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, elimu ya ufugaji wa samaki na viumbe wengine waishio kwenye maji ipewe msukumo mkubwa kwa vijana katika Halmashauri zote nchini.

Mheshimiwa Spika, nawatakia Mawaziri utekelezaji mwema wa majukumu yao ya kazi. Ahsante sana na naunga mkono hoja.