Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu wa watumishi wa Wizara kwa kazi nzuri. Changamoto zinazozungumzwa na Wabunge mkizifanyia kazi zikaungana na yale mazuri mnayofanya, hakika tutapiga hatua katika sekta hii kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara izingatie na kusimamia matumizi bora ya ardhi katika kutatua migogoro ya wakulima, wafugaji na wawekezaji kwenye Ranchi za Kitengule, Kikurula na Mwisa. Nashauri yafuatayo yafanyike:-

Mheshimiwa Spika, Wizara ikae na wawekezaji wa Kitengule na Kikurula Ranch akiwemo Super Doll na kuhakikisha mpango kazi wa matumizi ya ranchi yanaheshimiwa. Maelfu ya hekta zimetolewa Kitengule ila matumizi bora ya ardhi (ranchi ) hayazingatiwi.

Mheshimiwa Spika, interest yangu Mbunge na Wana Karagwe ni kuona wawekezaji kwenye Ranchi za Kitengule na Kikurula wanasaidia kutengeneza ajira kupitia matumizi bora ya ardhi (uwekezaji), wanachangia kipato cha Taifa (kodi na CSR) kwa kata zinazozunguka ranchi.

Mheshimiwa Spika, vikundi 25 vya Karagwe vya SACCOS za wafugaji, naomba sana vipate vitalu Mwisa II kuondoa migogoro ya ardhi kati yao na wakulima na wawekezaji niliowataja hapo juu.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Ufugaji cha Kikurula kimesahaulika, naomba Serikali ikisaidie ili kipate kipaumbele kwenye bajeti ya maendeleo na kiwe center of excellency kwa Kanda ya Ziwa. Ahsante sana.