Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, katika Soko la Samaki la Kimataifa la Dar es Salaam zaidi ya asilimia 75 ya samaki wanaouzwa pale ni samaki kutoka nje ya nchi. Jambo hili ni baya na linahitaji kuangaliwa upya ili tuweze kuwalinda wavuvi wa ndani. Kibaya zaidi wamiliki wa viwanda vya samaki ndio waagizaji wakubwa wa samaki kutoka nje.

Mheshimiwa Spika, zoezi la ukamataji nyavu za kienyeji maarufu kama makokoro linawaonea wavuvi wa samaki wadogo yaani dagaa kwa kuwa dagaa hawawezi kuvuliwa na nyavu nyingine tofauti na nyavu za macho madogo. Serikali iangalie uwezekano wa kuwapatia wavuvi wa dagaa nyavu maalum za kuvulia dagaa, maana bei yake ni kubwa na wavuvi wetu hawawezi kumudu.