Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika mitaa ya twitter, Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla anajulikana kama Mzee wa Nje ya Box kwa sababu ya falsafa yake ya kufikiri nje ya box. Sasa kwa kupewa Wizara hii, nafikiri sasa siyo tu afikiri acheze nje ya box kwa sababu ni Wizara ambayo inaweza kuitoa Tanzania, inaweza kuifanya Tanzania ikawa power house ya kiutalii kama ilivyo au inavyotarajiwa. Kwa bahati mbaya, amekaribishwa katika hatua mbovu kabisa, ameingia kwa mguu wa kushoto kwa maana kwamba bajeti yake anaingia tu imekatwa by 22 percent kiasi ambacho kinaonyesha Tanzania au Serikali kutokuwa na umakini au kutokuwa na nia ya kuona utalii unakua kwa kiasi kikubwa na hivyo anaanza kwa bajeti yake kupunguzwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, tunataka acheze nje ya box kwa sababu akicheza ndani haonekani. Kwa hivyo, Waziri muelezee Mheshimiwa Rais kama inawezekana ukicheza humu ndani hutafanya chochote. Lazima utoke kama walivyosema wengine uende kwenye maonesho, uende kwa matajiri wakubwa, utembelee nchi mbalimbali ndivyo ambavyo tutapata watalii. Kwa kufikiri tu nje ya box bila kucheza nje ya box tutabaki hapahapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia tunataka ututolee aibu ya nchi hii kwamba inatoa ajira 1,500,000 wakati ina uwezo wa kutoa ajira kubwa na nyingi zaidi. Nchi hii inapata watalii 1,300,000 wakati inaweza ikapata watalii hata milioni 2 na zaidi ikiwa kama Waziri atacheza nje ya box na siyo tu kufikiri ndani ya box. Pia nchi hii utalii unachangia asilimia 17 wakati tunaamini unaweza ukachangia hata zaidi ya asilimia 30 ikiwa Wizara hii itapewa umuhimu unaostahili na kwamba Waziri atapewa mamlaka na kuweza kufanya kazi yake vya kutosha na kuweza kufika mbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mauritius ina watu 1,500,000, watalii wanaopata ni 1,400,000 almost double ya raia wake, halikadhalika kwa Qatar, UAE na Seychelles ambayo inapata watalii 300,000 lakini raia wa nchi hiyo ni 100,000. Mtu anaweza akasema lakini wao ni kidogo lakini katika kupima kitu unapima kwa percentage ya watu au percentage ya kitu haijalishi kama wewe ni nchi kubwa au ndogo. Tanzania inapaswa kupata, kama mnavyoweka lengo zaidi ya watalii 3,000,000 lakini kwa kufikiri tu nje ya box hutafika mbali, cheza nje ya box. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu sera, tumekaa miaka 20 tangu sera iliyopita, sasa hivi najua kuna sera inatengenezwa kwa bahati nimeweza kuichungulia kidogo. Tumechelewa kufanya vitu vingi kwa sababu tumechelewa kurekebisha sera. Sera hii imetufanya tuwe nyuma katika vitu vingi ambavyo itabidi tutumie nguvu nyingi kuvirekebisha wakati tungeenda kwa wakati tungekuwa tumekwenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mengi niliyoona katika sera naona ina mwelekeo mzuri. Natarajia kwamba itakuwa shirikishi zaidi na tutakuwa na legislation nzuri na kutengeneza mazingira mazuri. Isipokuwa kitu kimoja sikukiona napenda kushauri nacho ni kuhusu lugha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sera hamkuzungumza suala la lugha. Kama tunataka kuvuta watalii wengi zaidi ni lazima hilo liwe muhimu. Kichina, Kirusi, Kituruki hizo ndiyo lugha ambazo zinakuja hivi sasa na wana raia wengi ambao wanaweza wakaja katika nchi zetu. Ningependa hili liingizwe katika sera kwa sababu linaweza kutusaidia kwa maana kwamba taasisi ambayo inafundisha utalii basi iwe na component ya lugha mojawapo katika major languages au coming major languages. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni kuhusiana na bombardier na utalii. Kumekuwa na dhana hapa ya kuamini kwamba tukiwa na bombardier maana yake tutakuwa na utalii, mimi siamini kwa sababu kuwa na ndege ni kitu kingine na kuwa na utalii ni kitu kingine. Unaweza kuwa na ndege lakini usiweze kui-brand vya kutosha kiasi ambacho tutaingia sisi tu Watanzania tukitoka Dubai tukija hapa au tukitoka Uingereza tukija hapa. Inachukua muda kwa watu kuamini brand ya ndege, muda sana na kwa hivyo mpaka brand ya bombardier iwe sawasawa pengine miaka mitano au miaka 10 mbele huko kama tutakuwa tunakwenda sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitawapa mfano mdogo tu, brand ya ndege ni shirika la nchi, wananchi wake wanapenda kujitambulisha. Chukueni mfano wa Kampuni ya Zantel na Zanzibar. Zantel kwetu sisi Wazanzibar ni brand yetu sisi Wazanzibar, pamoja na maudhi yake yote ya Zantel lakini Wazanzibar wote hapa lazima watakuwa Zantel halafu watakuwa na simu nyingine. Haiwezekani kuna Mzanzibar hana hata simu moja ya Zantel kwa sababu ni ndani ya moyo wake. Kwa hivyo, ukitaka raia wa nchi nyingine aipende bombardier, aje kwa bombardier ni lazima ujue kwamba kuna mapigano ya kupigania routes, alignment ya mtu kama mwananchi kwamba anaipenda nchi yake na kwa hivyo lazima asafiri na ndege ya nchi yake, kwa hivyo, itachukua muda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mmoja, Seychelles walikuwa na Air Seychelles ilikuwa inakwenda Dusseldorf kuingia Ujerumani, ni kituo pale cha utalii cha kupata mashirika makubwa ambayo namshauri Mheshimiwa Waziri charters ndiyo muhimu kuzitumia zile kuleta watalii. Wamekata kwenda Dusseldorf basi ule mwaka waliokata ndiyo watalii wametoka 16% mpaka 29% pamoja na kwamba Air Seychelles haendi Ujerumani. Kwa hivyo, is not about kwamba wewe una ndege yako ya Taifa ndiyo kupata watalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine nachotaka kuzungumza ni kuhusiana na brand. Leo Mheshimiwa Waziri umetuambia kuwa tutakuwa na hashtag ‘Tanzania Unforgettable’, nimeipenda kwa sababu ile motto ni nzuri na inaweza kuwa na maana ya kusaidia. Nimei-tweet leo na tayari kuna tweet nyingi zinasema kwamba kuwa na hiyo motto siyo issue, issue ni namna ya kui-brand sasa mpaka ikubalike. Kwa hivyo, it takes a lot of money ku-brand motto hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukifikiri Singapore, Malaysia au India Incredible India zimechukua a lot of money ku-invest. Kama leo hatuwezi kutenga pesa ya kutosha kuweza ku-invest katika brand zetu itabakia vilevile tu haitakuwa na maana yoyote ku-change from Tanzania Land of Kilimanjaro and Zanzibar na kuingia katika motto hii.