Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019; na Mapendekezo ya Serikali Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019; na Mapendekezo ya Serikali Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Labda nianze kwanza kwa kumkumbusha Mheshimiwa Selasini, wale anaowasema wale ndiyo shemeji zake wakubwa maana dada zake wana rangi ambayo inavutia sana makabila ya wale anaowasema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo hata nyumbani kwangu leo nimeondoka asubuhi nimewaaga wajomba zake. Kwa hivyo, haya mambo hayawezekani katika nchi yetu. Sisi ni wamoja na hata Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe ana wajomba zako wa kutosha, Mheshimiwa Mwigulu, Mheshimiwa Makamba and the list goes on and on! Huwezi kuzungumza ukabila Tanzania. Tuachane na haya mambo ya hovyo hovyo, hayatusaidii kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, naomba nianze kuchangia kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshiimwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa jinsi ambavyo anaendelea kutoa dira na mwelekeo wa Taifa letu katika kuboresha maisha ya Watanzania na kuleta ustawi wa Watanzania wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba nichangie hoja iliyotolewa na Mheshimiwa Richard Phillip Mbogo kuhusiana na uvunaji wa mazao ya maliasili kutoonekana kuchangia kikamilifu katika pato la Taifa letu. Alipenda kujua sababu hasa ni nini?

Mheshimiwa Spika, Sekta ya Misitu inachangia pato la Taifa kwa kiwnago cha asilimia 3.5 tu! Kinaonekana ni kiwango kidogo sana na hata sisi tunaosimamia sekta hii tunaona kwamba kiwango hiki ni kidogo, lakini kiukweli kiwango hiki hakipaswi kuonekana kidogo ila kinachosababisha kikubwa ni formula ya mfumo wa fedha kwa namna ambavyo mchango wa Sekta ya Misitu unakokotolewa, lakini mchango wa Sekta ya Misitu na mazingira kwa ujumla ni mkubwa sana kwenye uchumi wa Taifa letu kuliko ambavyo inasemwa kwamba ni asilimia 3.5 tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ku-mention mambo machache tu, Sekta ya Misitu inachangia kwenye upatikanaji wa maji, umeme na kwenye kilimo. Ukitaka kuitazama kwa upana wake utaona kwamba kama Watanzania zaidi ya asilimia 70 wanategemea kilimo kama shughuli yao ya msingi ya kiuchumi na kama kilimo kinategemea maji ya mvua na kama mvua zinatokana na uwepo wa misitu iliyohifadhiwa, maana yake kwa kiasi kikubwa sana uchumi wa Tanzania wa watu wetu walio wengi unategemea kwa kiasi kikubwa misitu ambayo inahifadhiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia, wanyama kuanzia ng’ombe au zaidi ya milioni 36 ambao Mheshimiwa Mpina kila siku hapa anajivunia nao wanategemea maji yanayotokana na uhifadhi wa vyanzo vya maji ambavyo ndiyo hiyo misitu inayohifadhiwa. Uzalishaji wa umeme, miradi ya umeme ambayo kila siku Mheshimiwa Dkt. Kalemani hapa anajivunia na Waheshimiwa Wabunge kila siku mnaomba umeme kwa ajili ya wannachi wetu. Ule umeme unaozalishwa kutokana na maji ukirudi kinyumenyume utakuja kugundua unatokana pia na uhifadhi wa misitu ambao tunaufanya katika Wizara yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, ukitaka kukokotoa vizuri ukaangalia hizo factor zote utaona wazi kabisa kwamba Sekta ya Misitu inachangia kwa kiasi kikubwa sana kwenye uchumi wa nchi yetu kuanzia kwenye kuzalisha umeme, kilimo, mifugo, samaki, uhifadhi wa wanyamapori kwa sababu kwenye hii misitu pia tunahifadhi wanyamapori. Sasa ni nani ambaye ana formula ya kiuchumi ya kuangalia umuhimu wa misitu katika uhifadhi wake wa bioanuai ambao unafanyika. Kwa kweli utaona ni kwa kiasi kidogo sana formula inayotumika na wenzetu wa Wizara ya Fedha kukokotoa umuhimu wa misitu inavyotumika.

Mheshimiwa Spika, pia misitu inatusaidia sana kuondoa madhara ambayo yangejitokeza kutokana na uwepo wa hewa ya ukaa. Kama tungekuwa hatuna misitu maana yake hewa ya ukaa ingeongezeka duniani na mazingira yangeharibika maradufu na maradufu. Kwa hivyo, kwa kuhifadhi misitu tunaweza kupunguza ongezeko la hewa ya ukaa angani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vile vile kwenye misitu tunapata asali, uyoga, dawa na tunapata hewa ya oxygen ambayo sisi sote tunaivuta. Sidhani kama formula za kiuchumi zinaangalia hadi oxygen ambayo tunavuta kila siku ambayo inatokana na uwepo wa misitu ambayo inatusaidia ku-control hewa ya ukaa hapa duniani.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, kwa kweli mchango wa misitu katika uchumi na katika pato la Taifa hauwezi kuwa ni hiyo asilimia 3.5 tu ambayo inazungumzwa na wanatakwimu za kiuchumi. Sisi tunaamini ingepaswa kuwa kubwa zaidi ya hiyo lakini kwa sababu ya formula inayotumika mchango wake unaonekana kuwa ni huo wa asilimia 3.5 ya pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, hoja ya pili nilipenda kuzungumzia ilitolewa na Mheshimiwa Magdalena Sakaya ambaye alisema kwamba utumiaji wa mazao ya misitu nchini kwa kutengeneza samani badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi ambapo tunapoteza chanzo cha mapato.

Mheshimiwa Spika, tunakubaliana na yeye, lakini bado sana teknolojia ya wazalishaji wetu hapa ndani imekuwa duni kwa kiasi kikubwa na mazao mengi yanayotokana na uvunaji wa misitu bado hayajatumika kikamilifu kwa matumizi mengine mbalimbali ikiwemo hiyo ya kutengeneza samani za maofisini na majumbani, lakini pia kutengeneza briquette kwa ajili ya mikaa na matumizi mengine mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Serikali imekuwa ikitoa maagizo mbalimbali mara kadhaa kuhusu taasisi mbalimbali za Serikali kuanza kutumia samani za hapa ndani na mfano mzuri ni kwenye Bunge lako ambapo tunatumia samani zinazotokana na mazao ya misitu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia mwaka huu kadri ambavyo Ilani ya Uchaguzi inatuelekeza tutenge asilimia 10 ya mazao ya misitu kwa ajili ya viwanda vya ndani, tunafanya hivyo. Huu ni mwaka wa pili sasa tumekuwa tukifanya hivyo, tunatenga uzalishaji kwenye misitu kwa asilimia 10 kwa ajili ya viwanda hususan katiak mashamba yetu ya Longuza na mashamba ya Mtibwa.

Mheshimiwa Spika, hoja ya mwisho ambayo napenda kuchangia inatokana na mchango alioutoa Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe hapa Bungeni kuhusiana na kwamba VAT imepunguza kasi ya ukuaji wa Sekta ya Utalii hapa nchini. Introduction ya VAT inaweza ikasemwa kwamba imepunguza kasi ya ukuaji wa Sekta ya Utalii lakini sisi tunapenda kuona kwamba bado ni mapema mno kufanya tathmini ya aina yoyote ile kama introduction ya VAT imeathiri ukuaji wa sekta ama la!

Mheshimiwa Spika, hatupingi wala hatukubali, lakini tunaona tu kwamba muda wa kufanya tathmini bado hautoshi na sisi tunaona sababu za ku-introduce VAT kwenye Sekta ya Huduma za Utalii ilikuwa ni ya maana sana, kwamba sekta hii kwa muda mrefu imekuwa ikionekana kama vile ni sekta ipo na haizalishi sana kwa ajili ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, sasa, ili Watanzania wa kawaida waweze kufaidika na Sekta ya Utalii ni lazima Sekta ya Utalii itozwe kodi ili hizo kodi ziende kutumika kutekeleza miradi ya kijamii ambayo itawagusa wananchi wengi, hilo ni jambo la kwanza. Pia, ni lazima wananchi wawezeshwe kushiriki katika Sekta ya Utalii ili nao wapate kipato kutokana na sekta yenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kwa bahati mbaya sana, sekta hii kwa miaka mingi imekuwa ikiwa controlled na wawekezaji kutoka nje ambapo mawakala wapo nje ya nchi na baadhi ya mawakala wapo ndani. Malipo kwa kiasi kikubwa yamekuwa yakifanyika nje ya nchi na kwa hivyo hapa Tanzania tunakuwa hatupati chochote. Pia wafanyabiashara wa Tanzania walikuwa wachache kwa miaka mingi.

Mheshimiwa Spika, sasa tulichokifanya katika miaka hii ni kutanua wigo wa kuwavutia wawekezaji wa ndani nao washiriki kwenye biashara ya utalii ili pia tuweze kupata kodi. Pia tunapo-introduce VAT maana yake walau tunapunguza economic leakage ambayo ilikuwa inasababishwa kwa mapato ya utalii kubaki nje na kutokuingia hapa ndani kwa sababu tunachaji kwenye huduma ambazo ziko hapa ndani. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa tuna uhakika sasa ule mchango mkubwa ambao unaonekana kwa sekta pana ya utalii wa asilimia 17.6 kuwa na faida kwa wananchi wa kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja na ahsante.