Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Naomba nianze kabisa kwa kusema kwamba mimi hapa si kawaida yangu kukamata shilingi lakini katika hili ninaanza nalo kabisa.

Mheshimiwa Waziri Dkt. Kigwangalla anafanya kazi nzuri na kwa utaalam. Mimi najua kwamba yeye ni Doctor of Medicine daktari wa binadamu, sasa daktari wa binadamu napenda kuamini kwamba kitu muhimu kuliko vyote kwake itakuwa ni kuliunda maisha ya binadamu. Sasa hali halisi katika hifadhi zetu kwa kweli namuangusha Mheshimiwa Waziri huyu ambaye tuna matumanini naye makubwa Kwa sababu hali ya hifadhi haijakaa vizuri.

Mheshimiwa Spika, tutakuwa tunajidanganya katika taifa hili ambalo kwa kweli linaongozwa na Mheshimiwa Rais anayesifika dunia nzima kwa kutetea wanyonge sasa watu/ majirani wa hifadhi si wanyonge? Maana yake ukweli ni kwamba hadi tunapozungumza sasa hivi kuna sintofahamu karibu na vijiji jiraniya hifadhi, mapori ya akiba na game controlled areas kwa kweli hali yao sio nzuri, na ni wajibu wa sisi Wabunge kuyasema mambo kama yalivyo kusudi Serikali mpate taarifa muweze kuyafanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka juzi Mheshimiwa Mama Samia Suluhu kwa mfano alisitisha zoezi la kutoa mifugo kwenye hifadhi kusudi Serikali ijipange watafute maeneo ya wafugaji. Suala hili halikufanyika; kwa hiyo maafisa wanyamapori na ninazungumza jambo ambalo nalijua kabisa, maana mimi katika jimbo langu Muleba Kusini tuna mapori ya Biharamulo, Buligi, Kimisi na kadhalika. Yanatokea kule kwa kweli wananchi hawawezi kutuelewa yasipofika katika Bunge hili na ninavyosikia taarifa za Tarime na kwingineko hali si nzuri; sasa tatizo ni nini na tufanye nini?

Mheshimiwa Spika, mimi ushauri wangu kwa Mheshimiwa Waziri ni kwamba atambue kwamba dhana ya misitu ya akiba iliyo nyingi imepitwa na wakati kwa Mkoa wa Kagera, naomba kabisa Mheshimiwa Waziri utakapokuja hapa utueleze una programu gani ya kuendeleza utalii, misitu na hifadhi katika mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kwamba kule achana na dhana ya Mapori ya Akiba ya Biharamulo na Kimisi na Buligi tangaza national park. Ukituletea programu ya kutangaza national park utakuwa na comprehensive program ya kufanya kazi na kuondokana na matatizo tuliyonayo sasa hivi, kwa sababu hizi shoroba ambazo nasikia mnaziweka hiyo ni kazi ya Mheshimiwa Waziri wa Ardhi. Tatizo linatokana na watu wa maliasili kujipimia ardhi, hamna mamlaka hayo, mimi najua na nilikuwa Waziri wa ardhi miaka mine, hayo mamlaka hamna. Tatizo linaanza kwa watu wa maliasili kuchukua kazi za surveyor ambaye yuko Wizara ya ardhi wanajipia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitatoa mfano, hapa Kisarawe kuna msitu wa Kazimzumbwe imekuwa ni mtafaruku mkubwa sana kwa sababu walikosea wale watu wa Maliasili, wali- shift mpaka na Gurumeti ni hayo hayo.

Mheshimiwa Spika, sasa nataka kusema kwamba kusudi tuende mbele, Mheshimiwa Waziri Kigwangala mimi nina imani naye lakini sasa hivi nimemkumbusha fani yake kwamba wajibu ni kuanza kulinda maisha ya binadamu. Sasa hatuwezi kukubalika tukionekana kwamba tunalindaje raia wetu.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nishauri kwamba kwanza tu-certify mipaka na Waziri wa Ardhi amsaidie Waziri wa Maliasili ku-certify mipaka tujue hifadhi ni nini na wanyama hawa lazima wapate maji. Kwa mfano pale Serengeti kuna sehemu kwamba Serengeti haifikii Ziwa Victoria, shoroba za wanayama kufikia maji nazo ni muhimu. Nimesema kwa mfano kule Nyakabango kuna ushoroba kati ya Chato na Muleba kule kwangu tumeweka ushoroba wakati wa kiangazi lazima nyati waende kunywa maji kwenye ziwa.

Mheshimiwa Spika, sasa unaweza ukakuta njia kama hizo za wanyama zinawekwa, lakini ziwekwe kwa mujibu wa sheria na si kwa wanyamapori kupima mipaka kwa macho. Kwamba wanakaa hapo wanaamua kama mpaka unapitia hapa unapitia pale.

Mimi naomba kusema kwamba tuna hifadhi kusudi tupate mapato. Sisi kwa upande wa Kagera programu tunayohitaji sasa tunataka national park ili na sisi tuweze kupata watalii, maana sasa hivi wale maafisa wanyamapori wako mule wanachoma mkaa tu wala hakuna hifadhi yoyote utakayoweza kukamilisha. Unatoa mifugo, watu wanahangaika, lakini wale wanaendelea na biashara ya mkaa, kwa hiyo unakuta kwamba mazingira yanazidi kuharibika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nataka kusema kwamba jambo hili ninaposema natoa shilingi naamini kwamba tunaweza kupata sasa mkakati wa kuendeleza kwa mfano upande wa Kagera tuna mifugo mingi.

Mheshimiwa Spika, hii tabia mbaya kila mtu anaitwa Mnyaruanda, Mganda, Mnyamkole, Mkenya, Mloita kama ni Wamasai wanasema wewe ni Mloita, kwa hiyo, ukienda kule Loliondo wanasema huyu ni Mloita huyu, ukienda Tarime unakuwa Mkenya, ukija Kagera kama mimi ndio Mnyamlenge asili. Sasa mambo hayo hayawezi kujenga Taifa hili, Taifa hili ni makabila mbalimbali na si dhana ya viongozi wa nchi hii wala chama tawala ninavyokielewa mimi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilitaka kusema kwamba tuenda scientifically, twende na programu na nishauri kwamba tuachane na biashara ya operesheni, hizi operesheni hatuna maslahi nazo, ni mabo ya kushtukiza ni mambo ya haraka na unakuwa huna proper program. Kwa hiyo nimeona niyaseme haya yawe on record.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nataka kusema kwamba ninaposema tuwe na development program zitaondoa matatizo yote haya na wafugaji ambao kimsingi ndio problem kati ya hifadhi na wafugaji wapewe ardhi.

Mheshimiwa Spika, huwezi kuendeleza mifugo au utalii kama huna proper land demarcations. Sasa watalii kwa mfano wanapokuja kuangalia wanyama ndani ya hifadhi wanaona na watu wanachunga ng’ombe, hiyo nayo haitusaidii, inaweza ikafukuza watalii.

Mheshimiwa Spika, wanakuja kuangalia simba, nyati na faru, that is granted, lakini sasa hawa watu ambao wafugaji ardhi zao ambazo wametengewa ziko wapi? Tangu mwaka juzi, Serikali hii ya Awamu ya Tano naishukuru sana walitoa miezi kumi kwa Mawaziri kadhaa hapa kutafuta ardhi za ufugaji, hiyo kazi haikufanyika kilichotokea watu wakaja kuondolewa kwenye hifadhi kama operation na kwa kweli kwa mateso makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, niseme pia na niwe on record, ni utawala wa sheria. Kama mtu ameshinda mahakamani na unatakiwa arudishiwe mifugo yake ni lazima irudishwe, kama haipo lazima inunuliwe Serikali hapo ni lazima kuwajibika, ndiko kuwajibika kwenyewe huko, kuwajibika hakuwezi kuwa sehemu tu ya wananchi na Serikali nayo ni lazima iwajibike pale ambapo kosa limefanywa na watendaji wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Muleba Kusini naomba nitaarifu kama tabia hii iko sehemu nyingine, kwa upande wa Waziri wa Mambo ya Ndani lazima mtambue kwamba OCD maana yake ni Officer Command District, kwa hiyo officer wa Biharamulo OCD wa Biharamulo hawezi kuja kumkamata mtu wa Muleba bila OCD wa Muleba kujua kwa mfano. Kwa hiyo unakuta kwamba ni uvunjivu kunakuwa na ka-group la watu kanajiandaa kula rushwa na kutesa wananchi. Sasa jambo hili kwa sababu wananchi wengi hawaelewi sheria hii vizuri unashangaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi kwangu wametoka Biharamulo kuja kuwakamata watu katika kata zangu za Nyakabango, Karambi, unasikia kwamba tumekamatwa na watu wa Biharamulo watu wa Biharamulo watawakamataje bila kufika kwa OCD wa Muleba? Kwa hiyo, ni matatizo kama hayo ambayo kwa kweli ni lazima niseme ukweli, na msema ukweli ni mpenzi wa Mungu jamani. Kwa mantiki hiyo nasema kwamba tusiharibiane utawala bora kwa sababu ya wale tuliowaweka chini tunapokwenda sisi wanatupa taarifa nzuri. Mheshimiwa Waziri nakukaribisha uje Muleba ujionee mwenyewe.

Mheshimiwa Spika, mtu anatoka Buharamulo kuja kumkamata mwananchi tena Diwani, anakamatwa anapelekwa mahakamani anasumbuliwa kabisa yaani huwezi kuamini. Mimi nikienda kama Mbunge wanaponisimulia wakati mwingine hata na mimi nashindwa kuamini, kwamba hii haiwezi kutokea lakini ndivyo inavyotokea. Kwa hiyo, unakuta ni network ya watu kwa hiyo Mheshimiwa Waziri mimi suingi mkono hoja nangojea majibu ya Waziri, ahsante sana.