Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuchangia katika hoja hii. Kwanza napenda niunge mkono hoja hii na nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa kuandaa bajeti ambayo ni nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kupanga ni kuchagua Watanzania tumefika mahali tukipanga hiki tunalalamika tunasema kibaya, tukianza hiki tunasema hiki ni kibaya, lakini yote Watanzania tufike mahali tunapopanga tuchague wenyewe. Siamini leo hii kwa Tanzania hii tuweze kulalamika sana. Ukichukua mfano kama Tanzania uki-compre na Kenya Uganda nchi zinazotuzunguka hapa hivi. Ni nchi gani ambayo ina rasilimali nyingi na kila neema kama Tanzania. Lakini tuko nyuma kwa sababu tukipanga kitu tunaanza kupinga tena tunakataa. Unataka uchumi wa viwanda unasema hutaki stiegler’s Gorge, tunataka umeme sijui wa aina gani na kadhalika. Tunakwenda wapi? Tunatoka wapi? Kama nchi lazima tuwe national agenda ya pamoja lakini tunakuja hapa tunaanza kuchukua mawazo ambayo hayatusaidii kama nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesikiliza mijadala yote hapa lakini nasema Watanzania lazima tubadilike kama tunapenda nchi hii lazima tukubali na kwenye mabadiliko lazima wengine waumie. Huwezi kuwa na mabadiliko katika nchi yoyote ile watu wasiumie haiwezekani. Nchi zote ambazo zimeendela watu waliumia sana, sana. Naomba Watanzania na hasa Wabunge sisi Wabunge humu ndani tusiwe ndumila kuwili. Kama tumekubali ajenda ya uchumi wa viwanda twende nayo tutoke nayo. Mnataka baada ya miaka mitano au kumi tufeli tuanze na ajenda gani nyingine tena. Let be serious. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Spika, amelenga penyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niendelee, kama tunataka utalii katika nchi hii lazima Bodi ya Utalii tuiwezeshe. Haiwezekani tukawa tunaongea ngonjera, utalii, utalii bila kuwezesha Bodi ya Utalii haiwezekani. Lazima kuwe na synergy ya mambo ambayo yanafanyika kama Taifa. Ningeomba sana kwa sababu ya muda sijui nitaongeaje sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo tunataka utalii huu uchochee uchumi wa nchi hii, lakini pamoja na haya lazima tuangalie kuna vitu ambavyo naomba sana Mheshimiwa Waziri uangalie sana hili. Nchi yoyote katika uchumi uweze kuwa vibrant lazima kuwe na biashara zinazofanyika. Watalii waingie hapa kwa gharama ndogo lakini wanakuja ku-spend zaidi hapa wanaingiza uchumi wetu hapa hivi.

Leo hii ukienda Dar es Salaam kwa mfano mahoteli yako tupu, ukienda Mwanza mahoteli yako tupu, ukienda Arusha mahoteli yako tupu. Sasa unasema watalii wanaongezeka, tunajiuliza swali kubwa sana kwamba tunafanyaje. Tuwe na mkakati wa Taifa tuondoe gharama ambazo zinakwaza watalii wasiingie hapa, tuchocheze ili watalii waweze kuingia na tuitangaze nchi yetu kwa urahisi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia gharama za mtu kuingia hapa nchini na kufanya kazi ni kubwa mno, dola 3050 ni hela nyingi sana za Kimarekani kama milioni saba za Tanzania. Hivi kweli biashara gani zinaweza ku-support mambo kama haya. Naomba mambo kama haya Waziri wa Fedha na wadau wengine wote tuongee kama nchi. Tusiongee kama mtu au kama Wizara kwa Wizara in isolation tufanye kazi kwa mtiririko ambao unaunganisha mambo. Lengo la nchi hii bila kuwa na uchumi hatuwezi kusonga mbele, bila kuwa na mapato ya kutosha hatuwezi kusonga mbele na bila utalii ambao ndiyo moja ya kigezo cha kutengeneza mapato katika nchi hii kuongezeka hatuwezi kupata mapato ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii.