Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Awali ya yote nipende kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake wanafanya kazi vizuri sana na nipende kusema Waziri na Naibu wake ni wasikivu na wanyenyekevu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachotaka kukuomba Mheshimiwa Waziri ile speed uliyoanza nayo wakati unateuliwa naamini umejipumzisha kidogo mara baada ya kutoka hapa ukaendelee nayo ile ile dhidi ya haya malalamiko yanayotolewa hapa ya askari wako kuuwa watu na kuliza watu, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu kingine ambacho nataka kusema tunapozungumzia utalii ni international business ni biashara ya kimataifa. Tuna vivutio vingi tunachangamoto ya miundombinu. Niliuliza swali last week linalohusiana na urithi wa malikale kule Kilwa Kisiwani hapaendeki hakuna kivuko cha uhakika hakuna miundombinu ya kueleweka. Kwa hiyo, niombe sana hii changamoto ya ufinyu wa bajeti ama huku kupunguzwa kwa bajeti kwa asilimia 22 ni tatizo, tuwaongezee bajeti kwa bahati nzuri tunapozungumzia Wizara ya Maliasili na Utalii kuna mashirika ya kimataifa ambayo yana-support wizara hii au sekta hii lakini pia tuiombe Serikali suala zima la miundombinu ya maeneo husika liko kwenye mikono yenu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu kingine nilichotaka kusema kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wake wa tano alisema malengo ya Wizara yanaendeshwa kupitia sheria, kanuni, taratibu na mikakati. Baadhi ya sheria kwenye wizara hii zimepitwa na wakati. Nikuombe sana Mheshimiwa Waziri uangalie namna bora ya kwenda kuzifanyia marekebisho Sheria ya Malikale lakini pia Sheria ya Masuala mazima ya Utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine sambamba na hilo ni kuhusiana na suala zima la Sera. Sera ya utalii ya mwaka 1999, Sera ya Malikale na Sera ya Utamaduni hebu tuziangalie hizi sera tuone kama tunaenda nazo vile ambavyo zilivyoandikwa. Sera zinasema katika kila Mkoa na kila Wilaya tuwe na cultural centre, lakini katika uhalisia hivyo vitu havipo. Kwa hiyo tuangalie matakwa ya sera hii kama bado tunaenda nayo na kama yako vinginevyo basi tuende tukazifanye kuzipitia upya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine Serikali imehamia Dodoma. Dodoma sasa hizi ni Jiji na hatuna museum hapa Dodoma na tutapokea wageni wengi sana kutoka mataifa mbalimbali na wenzetu kati ya vitu ambavyo wanavipendelea mara baada ya kazi ni kujifunza tamaduni mbalimbali ama kujifunza historia ya eneo husika. Kwa hiyo, niishauri Serikali ione umuhimu wa kuanzisha museum hapa Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine twende Pwani kidogo, Mheshimiwa Dau jana alizungumza kwa masikitiko ya hali ya juu kuhusiana na viboko wanaouwa watu. Lakini pia kule Kisarawe kuna mamba wanaokula watu. Niombe sana Wizara ya Maliasili na Utalii muende mkavune mamba wale, muende mkavune viboko wale kwa sababu itakuwa ni wazuri kwa masuala ya utalii. Kule waliko Kisarawe Mafidhi na kule waliko Mafia wanasababisha madhara makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda naomba tumalizie na maporomoko ya Mto Njombe. Maporomoko ya Mto Njombe…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.