Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa maelezo mafupi juu ya masuala mawili ambayo ni kero katika utendaji wa watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii. Moja ni hili la Wizara kuongeza maeneo ya hifadhi kwa kutwaa ardhi ya wananchi bila kufuata utaratibu. Binafsi suala hili naliona ni suala la kiuonevu sana kwa wananchi wa vijijini. Inasikitisha sana kuona sasa wanyamapori wanapewa kipaumbele na thamani kubwa kuliko wanadamu/raia wa nchi hii.

Mheshiwiwa Spika, suala la pili, ni mahusiano mabaya baina ya wahifadhi, wananchi na wafugaji wanaoishi jirani na mbuga. Sote ni mashahidi kuwa hali ya malisho ya mifugo ni changamoto kubwa kwa wafugaji wa Tanzania na Wizara ya Mifugo haijafanya jitihada kidhi kusaidia wafugaji kuzalisha malisho ya kutosha.

Suala la askari wanyamapori kukamata, kuswaga na kushikilia mifugo ya wafugaji katika hifadhi, kuwapiga risasi na kuwaua ng’ombe wanaowashikilia ni suala la kifedhuli na dhuluma. Askari wenu hufikia maamuzi hayo ya kukamata ng’ombe kwa misingi ya rushwa kuliko uhalisia. Mifugo ni maisha ya wafugaji. Unaposwaga na kushikilia mifugo ya wafugaji, kuiua na kuitelekeza bila huruma ni kuwafilisi na kuwatia umaskini wafugaji. Naomba Serikali itazame upya mambo haya ili kupunguza kero kwa wananchi na kuboresha mahusiano baina ya uhifadhi na wananchi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.